Mgomo

Wahudumu wa afya kuanza mgomo wao saa sita usiku kwa ajili ya mzozo wa kupandishwa daraja

Tishio kwa afya ya umma wakati huu wa janga la covid 19

Muhtasari

 

  •  Hakutakuwa na ukaguzi wa walio na virusi vya corona katika maeneo ya mipakani 
  •  Wamesema baadhi yao wamesalia katika nafasi moja kwa miaka zaidi ya 15 

 

Peterson Wachira ,mwenyekiti wa muungano wa maafisa wa Kliniki

 Huduma katika hospitali za umma huenda zitalemazwa kuanzia saa sita usiku wa kuamkia alhamisi .

 Hii ni baada ya wafanyikazi wa sekta ya afya kutishia kuanza mgomo wao  ili kulalamikia walichokitaja kama  kufeli kwa serikali kuu  kushughulikia lalama zao  kuhusu kupandishwa vyeo.

 Mgomo huo utavuruga utoaji wa huduma katika vituo vya afya katika viwanja  vya ndege  , vituo vya mipakani   hospitali ya kushughulikia majeraha y auto wa mgongo

 Hospitali nyingine zitakazoathiriw ana mgomo huo ni  Mathari , Othaya  , Benki ya kitaifa ya damu  ,maabara za umma na vituo vuote vya afya vinavyohudumiwa na wafanyikazi wa wizara ya afya .

" Ni bahati mbaya sana kwamba wakati huu wa janga la corona tunawapa habari hizi mbaya .hakutakuwa na vipimo vya Covid 19  katika maeneo yote ya kuingia nchini’ amesema   mwenyekiti wa muungano wa kitaifa wa  maafisa wa kliniki Peterson Wachira .

" Tumelaghaiwa hapo awali  mara kadhaa  na hatutakubali mtido huo kwani sisi sio watoto’

 Miungano mingine itakayohusika na mgomo huo ni muungano wa kitaifa wa wauguzi ,muungano wa wahudumu wa afya  ,maaafisa wa maabara kote nchini ,muungano wa kitaifa wa wanafamasia   na wahudumu wa sekta nyingine za afya .

 Miungano hiyo imesema kwamba ni jambo la kuwaondoa motisha  kwamba wizara ya afya kwa miaka mingi imeahidi  kutekeleza mpango wa kuwapandisha vyeo na ngazi kazini lakini imekuwa  ikitumia njia za kuchelewesha ahadi hizo .

 Kwa sababu ya hatua hiyo baadhi ya wanachama wao wamekuwa katika ngazi moja ya kazi kwa Zaidi ya miaka 15