BBI

Cherargei amtaka Uhuru kuunda kamati mpya ya BBI kukusanya upya maoni ya wakenya

Kamati mpya inafaa kukusanya maoni

Muhtasari

 

  • Matamshi yake yanajiri  baada ya rais Uhuru na Raila kulegeza misimamo yao kuhusu kurekebisha baadhi ya mapendekezo katika ripoti ya BBI .
  • Cherargei amesema  kamati mpya ya  usimamizi wa mchakato wa BBI  inafaa kuwa na uwezo wa kushughulikia masuala yote ynayoibuka  kutoka sekta zote  na matabaka ya watu

 

Seneta wa Nandi Samson Cherargei

Seneta wa Nandi Samson Cherargei  amemshauri rais Uhuru Kenyatta kuunda kamati nyingine mpya ya BBI  ili kukusanya maoni ya wakenya .

 Seneta huyo amesema  kuwasilisha mapendekezo kwa kiongozi wa ODM Raila Odinga sio hakikisha kwamba marekebiusho hayo yatawekwa katika ripoti ya mwisho .

 Matamshi yake yanajiri  baada ya rais Uhuru na Raila kulegeza misimamo yao kuhusu kurekebisha baadhi ya mapendekezo katika ripoti ya BBI .

 “ Makundi haya yametoa mapendekezo ya kuirekebisha ripoti hiyo ,wataapeleka wapi?’ Cheraragei  amehoji

“ kwa maoni yetu tunamtaka rais atumie kasi kuunda kamati nyingine ya BBI  ili ifanye kazi ya kukusanya mapendekezo ya wakenya . Kuwasilisha maoni hayo kwa kiongozi wa ODM sio jambo linalofaa kwa sababu hana uwezo wa kuyajumuisha yote katika ripoti ya mwisho kama inavyofaa’

Cherargei amesema  kamati mpya ya  usimamizi wa mchakato wa BBI  inafaa kuwa na uwezo wa kushughulikia masuala yote ynayoibuka  kutoka sekta zote  na matabaka ya watu .

  Seneta huyo amesema marekebisho ya katiba ni jambo ambalo linafaa kuwahusisha watu wote  na halifai kuingizwa siasa .

 “ Nimefurahi kwa sababu  kuna fursa ya kutoa  mapendekezo . baadhi ya viongozi hata bungei walikuwa wametuambia kwamba hakuna hata koma itakayoongezwa au kutolewa katika ripoti hiyo’

 Siku ya jumatatu Raila alikutana na viongozi kutoka jamii ya  wafugaji wa kuhama hama  wakiongozwa na waziri wa Fedha Ukur Yatani  na baadaye wakasema wataiunga mkono iwapo baadhi ya sehemu zitabadilishwa