Mkasa wa moto

Wafanyibiashara wapata hasara baada ya moto kuzuka tena Gikomba

Kisa cha leo ndicho cha hivi punde gIKOMBA

Muhtasari
  •  Moto huo ulianza ijumaa alfajiri 
  •  wafanyibiashara na zima moto wanaendelea kukabiliana na moto huo

 

 Wafanyibiashara katika soko la  Gikomba wanakadiria hasara kubwa waliopata baada ya moto mwingine kuzuka na kuteketeza sehemu ya soko hilo ijumaa alfajiri . maafisa wamesema chanzo cha moto huo hakijulikani . wafanyibiashara wameendelea kuuzima moto huo  ulioanza  mida ya alfajiri .

  Zima moto kutoka kaunti ya jiji la nairob pia zimeelekea katika eneo hilo kusaidia katika juhudi za kuuzima moto huo.

 Kumekuwa na msururu wa visa vya moto kuzuka katika soko hilo  na kuwasababishia wafanyibiashara hasara ya mamilioni ya pesa .

  Mnamo februari Mosi  moto mwingine uliteketeza sehemu kuba ya soko hilo  na kuwaacha hoi mamia ya wafanyibiashata . maafisa wa kaunti wameapa kufanya uchungiuzi kufahamu chanzo cha mikasa hiyo ya moto