Siasa

Aukot Nje: Msajili wa vyama aidhinisha kuondolewa kwa Aukot kama kiongozi wa Thirdway

Aukot aliinda kufika mbele ya kamati ya nidhamu

Muhtasari

 

  •  Anashtumiwa kwa kutumia vibaya pesa za chama na kukosa uwazi
  •  Aukot hata hivyo atasalia kuwa manachama wa Thirdway Alliance 

 

Ekuru Aukot

Msajili wa vyama vya kisisasa ameidhinisha kuondolewa kwa Ekuru Aukot kama kiongozi wa chama cha  Thirdaway Alliance.

 Katika barua ya tarehe 18 Novemba mwaka huu  iliyoandikiwa katibu mkuu wa chama hicho  Fredrick Okango,  msajili wa vyama  Ann Nderitu  amesema ofisi yake imeridhishwa na  utaratibu wa kumuadhibu Aukot na kuondolewa kwake kutoka nafasi hiyo .

  Amesema  “ Chama  kinashauriwa kutekeleza  uamuzi wa baraza kuu kama inavyokubaliwa chini ya kipengee cha  14(k)  cha katiba ya chama .

 Hata hivyo Nderitu amesema uamuzi wa kumfurusha Aukot kama mwanachama haujaridhisha ofisi yake  na hivyo basi kudinda kuishinisha uamuzi huo .

Aukot  alifurushw akutoka chama hicho mwezi septemba  kwa utumizi mbaya wa fedha  na ukosefu w uwazo kwa  wanachama wa Thirdway Alliance .

NE iliamua kumuondoa Aukot kama kiongozi wa chama hicho alipokataa kufika mbele ya kamati ya nidhamu .