- Ruto amesema jaribio hilo la Kinoti ni la kuzua uhsama wa kikabila
- washirika wa Ruto wamemkashfu Kinoti kwa kukubali kutumiwa kisiasa
Naibu wa rais William Ruto ametoa msimamo wake kuhusu kufufuliwa kwa kesi za ghasia za baada ya uchaguzi akisema ni njama ya kuleta ukabila
" Jaribio lenye hila za kuzirejesha kesi hizo ni njama ya kufufua tena mradi wa ukabila’ amesema
Kupitia twitter amesema ,mradi huo wa ukabila uliharibiwa na vugu vugu lake la mahasla baada ua kugunduwa kwamba umaskini na ukosefu wa kazi umesababisha na uongozi mbaya na sio makabila ya humu nchini .
Imeripotiwa kwamba serikali imeamua kuzifufua kesi za ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007/2008 huku waathiriwa wa kuteketezwa kwa kanisa la Kiambaa wakiwa tayari kutoa ushahidi .
Hatua hiyo imejiri miaka saba baada ya serikali kusema haina ushahidi kuwachukulia hatua wanaodaiwa kuteleleza mauaji , uharibifu wa mali na machafuko baada ya uchaguzi huo .
Wabunge Zaidi ya 40 wanaomuunga mkono naibu wa rais Ruto wamemkashifu vikali mkuu wa DCI George Kinoti kwa kuwa na nia ya kuzifugua kesi hizo .
Wabunge hao wa tanga tanga wamemshtumu Kinoti kwa kujaribu kuchochea ghasia miongoni mwa jamii zinazoishi Rift Valley .
The provocative INCITEMENT to ethnic hate/division INTENDED by the ressurection of PEV is an EVIL attempt to resuscitate the TRIBE project DESTROYED by the HUSTLER movements' REALISATION that poverty&unemployment DELIBERATELY bred by poor leadership is our PROBLEM NOT our tribes.
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) November 24, 2020
" Wanaomtumia Kinoti wamerejea ..ni wazi kwamba ana watu wanaomtuma kufanya hiki anachlenga kufanya kwa kuwatumia vibaya waathiriwa wa ghasia za uchaguzi ili kuendeleza ajenda ya kisiasa’ amesema seneta wa Nakuru Susan Kihika
Akiisoma taarifa ya wabunge hao ,Kihika amedai kwamba Kinoti anatumiwa kuwalazimisha wakenya kuunga mkono Ripoti ya BBI na kuthibiti siasa za urithi mwaka wa 2022 .
Hata hivyo Kinoti amepuuza madai hayo akisema kwamba halengi kuzifufua kesi hizo .amesema kikao chake jana ni kuwahakikishia waathiriwa wa ghasia hizo na wakenya kwamba hapatatokea visa kama hivyo tena na pia baada ya watu kadhaa kuripoti kutishwa .