HIV

Dawa ya HIV,DTG yahusishwa na kuwazidishia uzani wanawake

DTG inasalia kuwa dawa yenye ufanisi zaidi sokoni ya ARV

Muhtasari
  • Kenya  ilianzisha matumizi ya DTG  mwaka jana  ili kuziba nafasi ya dawa nyingine za ukimwi kama dawa msingi ya matibabu .
  •   Takwimu  kutoka tafiti mbili zilizofanywa  Kenya ,Afrika Kusini na Cameroun  zimeonyesha ongezko kubwa la uzani wa watumiaji wa dawa hiyo .

 Dawa mpya   ya HIV kwa jina  Dolutegravir  inakabiliwa na changamoto mpya baada ya utafiti kuonyesha kwamba inasababisha wanawake kunenepa .

 Pia haisaidii  kupunguza  virusi kwa watu ambao tayari miili yao ilikataa kukubali dawa nyingine za HIV .

 Hata hivyo  Dolutegravir, ambayo pia inajulikana kama DTG  inasalia kuwa dawa yenye uwezo zaidi  kukabiliana na virusi vya HIV  na mseto wake unapendekezwa  na WHO kwa watu walio na HIV .

Kenya  ilianzisha matumizi ya DTG  mwaka jana  ili kuziba nafasi ya dawa nyingine za ukimwi kama dawa msingi ya matibabu .

  Takwimu  kutoka tafiti mbili zilizofanywa  Kenya ,Afrika Kusini na Cameroun  zimeonyesha ongezeko kubwa la uzani kwa watumiaji wa dawa hiyo .

Utafiti wa kwanza uliofanywa na  African Cohort Study,  uliwahusisha watumiaji 2000 kati ya januari mwaka wa 2013 na  Novemba mwaka wa 2019  katika kliniki 12 zinazosaidiwa na  Pepfar- katika nchi za  Kenya, Nigeria, Tanzania  na Uganda.

 Watu waliotumia  mchanganyiko wa  Dolutegravir/TDF/Lamivudine walikuwa na uwezo wa asilimia 85  kuongeza uzani  kuwaliko waliokuwa wakitumia dawa zisizo na mchanganyiko wa   dolutegravir

 Vile vile wale waliokuwa chini ya matumizi yay a DTG  walikuwa  na uwezekano wa asilimia  27  kupata  hyperglycemia-mkurupuko wa sukari kupindukia katika damu unaohusishwa na maradhi ya kisukari .

  Katika utafiti wa Afrika kusini na Cameroun  iligunduliwa kwamba  wanaume waliokuwa wakitumia mseto wa DTG walipata ongezeko la uzani wa kilo tano .

 Wanawake waliongeza kilo  nne hadi   nane

 

DTG  inasalia kuwa dawa yenye ufanisi zaidi sokoni   ya  ARV

 Imesajili uwezo mkubwa wa matokeo ,ni rahisi kutumia  na ina athari chache za kando  ikilinganishwa na dawa mbadala ,kulingana na shirika la Afya Duniani WHO .

 Dawa hiyo  inatengezwa na  ViiV Healthcare, kampuni yenye makao yake nchini Uingereza ambayo inashughulika na dawa za kutibu HIV .

Asilimia 76 ya kampuni hiyo inamilikiwa na GlaxoSmithKline,  asilimia 13.5  na  Pfizer  na asilimia 10   na  Shionogi ya Japan.