Siasa 2022

Washirika wa Ruto wahamia chama kipya

Mgombeaji huru aliyeungwa mkono na Ruto alimshinda mgombeaji wa chama cha ODM baada ya Jubilee kukosa kumsimamisha mgombeaji kwa sababu ya mwafaka wa handshake

Muhtasari
  • Tulikihama chama cha Jubilee kitambo sana .Sasa tupo chama kipya’ amesema mbunge mmoja aliye karibu na DP Ruto  ambaye hakutaka  kutambuliwa
  •  Msajili wa vyama vya kisiasa siku ya jumatatu alitoa notisi ya nia ya kubadilisha jina la PDR  hadi UDA  na kuzua uvumi kwamba kambi ya Ruto imeshapata    njia ya kupata  chombo kipya cha kutumia kwa uchaguzi mkuu ujao endapo ataamua kuondoka Jubilee .
Naibu wa rais William Ruto

 Baadhi ya washirika wa naibu wa rais William Ruto  wamedai kwamba huenda akakitumia chama kingine kuwania urais mwaka wa 2022 .

  Wakizungumza siku ya jumapili wamesema kwamba hatua ya kukibadilisha jina chama cha  Party for Reforms and Development  hadi  United Democratic Alliance  ni sehemu ya mpango huo wa kuhakikisha kwamba Ruto anapata makao mapya akiamua kuondoka Jubilee .

 “ Tulikihama chama cha Jubilee kitambo sana .Sasa tupo chama kipya’ amesema mbunge mmoja aliye karibu na DP Ruto  ambaye hakutaka  kutambuliwa

 Msajili wa vyama vya kisiasa siku ya jumatatu alitoa notisi ya nia ya kubadilisha jina la PDR  hadi UDA  na kuzua uvumi kwamba kambi ya Ruto imeshapata    njia ya kupata  chombo kipya cha kutumia kwa uchaguzi mkuu ujao endapo ataamua kuondoka Jubilee .

 Katika arifa ya gazeti rasmi la serikali  iliyochapishwa siku ya jumatatu  ,chama hicho pia kinataka kubadilisha nembo yake  kutoka  fahali  ili kuwa wheelbarrow  na kauli mbiu ya ‘Kazi Ni Kazi’

Ruto na washirika wake wamejipata katika kipindi cha mvutano na uongozi wa chama cha Jubilee  hasa kuhusiana  na masuala makubwa kama vile kuwasimamisha wagombeaji katika chaguzi ndogo .huko msambweni  ,mgombeaji huru  aliyeungwa mkono na Ruto   alimshinda mgombeaji wa chama cha ODM  baada ya Jubilee kukosa kumsimamisha mgombeaji kwa sababu ya mwafaka wa  handshake