Sonko korokoroni

Sonko alala seli baada ya kuhojiwa na DCI

Mojawapo ya kisa hicho kinadaiwa kutokea katika shule moja ya watoto mtaani Buruburu mwaka wa 2019

Muhtasari
  •  Polisi wanatarajiwa kuwasilisha ombi la kutaka kumzuilia kwa muda wanapoendelea na  uchunguzi wao .
  •  Mojawapo ya kisa hicho kinadaiwa kutokea  katika shule  moja ya watoto mtaani Buruburu mwaka wa 2019
Sonko na mmoja wa mawakili wake George Kithi katika makao makuu ya DCI

 Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko  alilala seli jumatatu usiku  na anatarajiwa kufikishwa kortini siku ya jumanne ili kujibu mashtaka mbali mbali .

 Alichukuliwa  siku ya jumanne asubuhi kutoka kituo cha polisi cha Muthaiga  ambako alikuwa  amelala usiku wa  jumatatu  na kupelekwa katika  makao makuu ya DCI ili kuhojiwa .

Sonko,  alitumia muda  mwingi wa siku ya jumatatu katika afisi za DCI  kwenye barabara ya Kiambu  na anatarajiwa kufikishwa kortini baadaye leo .

 Maafisa wanaofahamu kesi yake wanasema atakabiliwa na  mashtaka saba ya wizi wa kimabavu na mashtaka matano ya  kujeruhi .

 Polisi wanatarajiwa kuwasilisha ombi la kutaka kumzuilia kwa muda wanapoendelea na  uchunguzi wao .

 Mojawapo ya kisa hicho kinadaiwa kutokea  katika shule  moja ya watoto mtaani Buruburu mwaka wa 2019

 Siku ya jumatatu makachero walimhoji Sonko kuhusu matamshi yake kuhusiana na ghasia za uchaguzi wa 2017 . Sonko hata hivyo alikataa kuanikisha taarifa akisema  amezuiwa na mahakama .

 Ni wakati huo ambapo Sonko aliarifiwa na polisi kwamba hatoachiliwa huru kwa sababu kulikuwa na mashtaka mengine dhiidi  yake .

  Mawakili wake  John Khaminwa, Assa Nyakundi, Evans Ondieki  na  George Kithi walikuwepo .

 Juhudi zao za kutaka Sonko aachiliwe kwa dhamana ziliambulia patupu . Sonko aliagizwa kufika mbele ya DCI baada ya kudai kwamba yeye na katibu wa kudumu wa usalama wa ndani Karanja Kibicho walihusika na kupanga ghasia wakati wa uchaguzi wa 2017 kisha kukilaumu cha  cha ODM kwa ghasia hizo .