Mauaji

Mwanafunzi wa chuo kikuu akamatwa kwa kuwachoma jamaa zake watatu usiku

Polsi walimkamata siku ya jumatatu

Muhtasari
  •  Wanakijiji wanasema mshukiwa awali alikuwa amelalamika kwamba wazazi wake wanampenda sana kakake kumliko na kutishia kufanya jambo ambalo hakulieleza .
  •   Kibuyu cha petroli ,kisu na tochi vilipatikana katika boma hilo .mkuu wa DCI  wa Mumias magharibi  Robert Muriithi  amekamatwa kwa uharibifu na  sio kwa mauaji .
Eugene Omonyore mwenye umri wa mika 23 aliyeuawa kwa kuteketezwa na kakake ,Mumias magharibi

Mwanafunzi wa chuo kikuu amekamatwa kwa madai ya kuwachoma kwa moto   kakake ,mke na mtoto wao katika kijiji kimoja huko Mumias ,kaunti ya kakamega .

Innocent Makokha anadaiwa kuichoma familia ya kakake katika nyumba yao huko  Eshikalame  wadi ya Musanda katika eneo bunge la mumias magharibi mapema siku ya jumamosi .

 Eugene Omunyore, 23,  mkewe  Miriam Echesa  na binti yao mwenye umri wa  mwaka mmoja unusu  walifaulu kukwepa kutoka nyumba yao iliyokuwa imeshika moto lakini walipata majeraha mabaya .

 Walikimbizwa katika hospitali ya  St Mary's Mission Hospital  mjini  Mumias ambako baadaye walihamishwa hadi Bungoma .  Omunyore alifariki siku ya  jumamosi ilhali binti yake aliaga dunia siku ya jumatatu .mke wake yungali  amelazwa akiwa katika hali mbaya katika hospitali ya   Life Care mjini Bungoma .

 Wanakijiji wanasema mshukiwa awali alikuwa amelalamika kwamba wazazi wake wanampenda sana kakake kumliko na kutishia kufanya jambo ambalo hakulieleza .

 Inadaiwa alirejea nyumbani siku ya jumamosi na kuanza kuchimba kaburi la kumzika kakake akizungumza lugh ambayo hakuna aliyeelewa . Kisha baadaye alipandwa na mori na kuanza kupasua  madiridha ya vioo katika boma lao  hatua iliyowafanya wazazi wake kuwaita polisi ambao walimkamata .

 Polsi walimkamata siku ya jumatatu

" Nilisikia ukemi  kutoka kwa wanangu wadogo wakitaka mlango ufunguliwe wakisema nyumba ya kaka yao ilikuwa ikiteketea .Nilipoamka niliona moto mkubwa  umeifunika nyumba ake na nikatoka nje’ amesema Sella Atsieno, mamake marehemu Eugene

Atsieno amesema mshukiwa alikuwa akigombana naye pamoja na kakake kila mara  na mara ya mwisho walipogombana ilikuwa siku nne zilizotangulia huku akiondoka baada ya kutoa onyo kwamba atafanya kitu kibaya .

 Omunyore alirejea siku ya jumamosi  baada ya kuwa nje kwa siku tatu  na kuanza kumtukana pamoja na waliokuwa kwenye boma wakati huo  huku akiwatishia kwa panga .Kisha alichukua jembe na kuanza kuchimba alichopsema ni kaburi  la kakake.

 Babake Omunyore  Apollo Kalio amesema ukemi na kelele ziliwavutia majirani walioanza kusaidia kuuzima moto huo uliosambaa katika nyumba hiyo ya vyumba viwili .

  Kibuyu cha petroli ,kisu na tochi vilipatikana katika boma hilo .mkuu wa DCI  wa Mumias magharibi  Robert Muriithi  amekamatwa kwa uharibifu na  sio kwa mauaji .