Wanabodaboda 16 walioshtakiwa kwa madai ya kumdhulumu dereva wa kike aachiliwa

Muhtasari

•Hakimu wa mahakama ya Milimani Martha Nanzushi  aliwaachilia 16 hao Jumatatu baada ya DPP kusema hawakupata ushahidi wa kutosha kuwahusisha na  kosa hilo.

•Mshukiwa mkuu wa tukio hilo Zachariah Nyaore Obadiah,  hata hivyo atashtakiwa leo.

James Mutinda Muema, Samuel Wafula Muswahili, Charles Omondi Were, Japheth Bosire Obano, Hassan Farah Forah na wengine kumi na mmoja mbele ya hakimu mkuu Martha Nanzushi wameachiliwa huru ambapo walishtakiwa kwa kumdhulumu mwanadiplomasia wa kigeni kwenye barabara ya Wangari Maathai mnamo Machi 28, 2022.
James Mutinda Muema, Samuel Wafula Muswahili, Charles Omondi Were, Japheth Bosire Obano, Hassan Farah Forah na wengine kumi na mmoja mbele ya hakimu mkuu Martha Nanzushi wameachiliwa huru ambapo walishtakiwa kwa kumdhulumu mwanadiplomasia wa kigeni kwenye barabara ya Wangari Maathai mnamo Machi 28, 2022.
Image: DOUGLAS OKIDY

Mahakama imewaachilia washukiwa 16 waliokuwa wamezuiliwa kutokana na video inayosambaa ya dereva wa kike akinyanyaswa  katika Barabara ya Wangari Maathai.

Hakimu wa mahakama ya Milimani Martha Nanzushi  aliwaachilia 16 hao Jumatatu baada ya DPP kusema hawakupata ushahidi wa kutosha kuwahusisha na  kosa hilo.

Upande wa mashtaka ulisema afisa wa upelelezi hakupata ushahidi unaowahusisha washukiwa hao na kesi ya unyanyasaji wa kijinsia mnamo Machi 4.

“Kutokana na afisa mpelelezi kukosa ushahidi wa kuwafungulia mashtaka watuhumiwa, ninawaachilia chini ya kifungu cha 87 (a) cha Kanuni ya Adhabu”, Hakimu aliamuru.

Aliagiza washukiwa warudishwe katika kituo cha polisi cha Gigiri ili  kuchukua simu zao na mali zao nyingine.

Mshukiwa mkuu wa tukio hilo Zachariah Nyaore Obadiah,  hata hivyo atashtakiwa leo.

Upande wa mashtaka ulisema wana ushahidi wa kutosha wa kumshtaki na Zachariah  katika kesi ya shambulio hilo.

Washukiwa hao walikuwa wamekaa rumande kwa zaidi ya siku 15 wakisubiri uchunguzi.