"Hadi sasa sijui wazazi wangu halali, hii ni kwa sababu wazazi wangu walikuwa wnataka kuniavya lakini yaya ambaye alikuwa ameandikwa kwetu alimkataza mama yangu
Alimwambia anizae na ampe mtoto, sijui kwanini au makubaliano waliokuwa nayo wakati huo, baada ya hapo nyanya huyo alinichukua na kuanza kunilea
Baada ya muda nyanya aliaga dunia na kuachwa katika chumba cha watoto mayatima, ilifika muda tukaambiwa hatupaswi kuwa katika eneo hilo
Baada ya muda nyanya aliaga dunia na kuachwa katika chumba cha watoto mayatima, ilifika muda tukaambiwa hatupaswi kuwa katika eneo hilo
Wale wengine walikuwa wanalelewa nami walichukuliwa nami nikaachwa nilienda kuishi mitaani." Alisimulia Leila.
Alizidi na kuzungumza,
"Kwa sababu sikuwa na chakula mwanaume mmoja alichukua fursa ya kunitumia ili nipate chakula hapo ndipo nilipata ujauzitoNilijifungua mtoto wa kiume, kwa niliishi mitaani na yeye nilikuwa nasaidiwa na watu kutoko msikitini na kanisani, watu walichukua nafasi hiyo kumhuzisha katika vitendo mbalimbali
Msikiti uliamua kumsomesha mtoto wangu kwa maana sikuwa na uwezo, kuna mwalimu ambaye alikuwa anajiita wa dini ambapo nilimkubali kijana wangu kujiunga
Lakini hayakuwa masomo ya dini mbali walikuwa wanafunzwa jinsi ya kuwa gaidi, katika kidato cha pili alibadilika ghafla na kuacha masomo
Hii ni kwa sababu nilikuwa nakula miraa, na hata kulewa watoto wangu wakiwa hapo, nilibarikiwa na mtoto mwingine msichana ambaye alikuwa anachapwa sana na ndugu yake baada ya kubadilika
Nilimuongelesha lakini siku moja aliamka na kuniambia anataka kuenda Somalia." Leila Alisimulia.
Baada ya kijana wake kubadilika Leila alienda kupata msaada kutoka kwa chifu ili kijana wake hasiweze kujiunga na kundi la Alshabaab.
Ilimbidi aende mpaka kwa serikali ili mwanawe abadilike, kijana huyo alifuatiliwa na serikali na mwishowe kubadilika.
"Baada ya kufuatiliwa nilimrudisha shule na kisha akamaliza shule ya upili, na nilimuokoa kwa sasa amebadilika na anaendelea vyemaNimewalea watoto wangu pekee kati ya vijana ambao waliokuwa na wao yeye tu ndio amesalia na kubadilika." Alisema.
Kwa mengi zaidi tembelea mtandao wetu wa kijamii wa youtube.