Mbunge wa Nyali Mohammed Ali amezichapisha picha za kituo kipya cha polisi cha Nyali kilichojengwa na pesa za mfuko wa hazina ya CDF ,anazosimamia . Moha Jicho Pevu kama anavyofahamika na wengi mitandaoni amesifiwa sana na wafuasi wake katika twitter alipoonyesha kazi ambayo ameifanya kama mwakili wa bunge wa eneo hilo .
Hata hivyo Wakenya ni watu wa kipekee, kuna waliomtaka asijizolee sifa za ufanisi wa ujenzi wa kituo hicho wakidai pesa zilizotumiwa ni za umma . Mgala muue lakini haki yake mpe jamani ,hapa Moha amefanya kitu kisafi sana !
Tazama maoni ya baadhi ya waliozungumzia mradi huo twitter
https://twitter.com/MohaJichoPevu/status/1229778836277071872