Hili limebainika baada ya Kithure kindiki wa Tharak Nithi, Kipuchumba Murkomen wa Elgeyo Marakwet na Samson Cherargei kutupilia mbali nyadhifa ambazo walikuwa wametengewa na chama hicho.
Kindiki ambaye alikuwa ameteuliwa katika kamati ya haki na sheria alitupilia mbali uteuzi huo akisema akili zake sasa zinaangazia tu utendakazi wake kwa wananchi wa Tharaka.
Kwa upande wa Cherargei ambaye alitimuliwa kama mwenyekiti wa kamati ya kuangazia sheria, alitupilia mbali wazo la kuteuliwa kama mmoja wa kamati ya Powers and Privileges .
“I hereby write no notify you that I have declined the appointment to be a member of the Powers and Privileges Committee in the Senate,” alisema Cherargei .
Murkomen, ambaye alitimuliwa kama kiongozi wa wengi kwenye bunge la seneti pia alikataa kuchukua wadhifa wa kuwa mwanachama wa kamati ya kuangazia ugatuzi nchini kama njia ya kuchukuwa nafasi ya seneta wa Laikipia John Kinyua.
“This afternoon I learnt from the media that I have been proposed to serve in the Senate Devolution Committee in effect replacing Senator Kinyua who is being punished for standing with me. Accepting the position will be tantamount to repaying unstinting loyalty with spite&treachery,” Murkomen aliandika.