Kamanda wa polisi katika kaunti ya Nandi Thomas Ngeiywo amehamishwa hadi makao makuu ya polisi wiki moja yake kushindwa kumzuia gavana wa kaunti hiyo Stephen Sang Kuvamia shamba la chai linalohusishwa na waziri wa zamani Henry Kosgey .
Bw. Ngeiywo alitakiwa kurejea Nairobi wiki jana na mrithi wake kuthibitshwa siku ya jumanne . Nafasi yake itachukuliwa na Samuel Ole Kine ambaye alikuwa katika makao makuu baada ya kutolewa Trans Nzoia .
Bwana Kine alihudumu katika wadhfa kama huo kabla ya kuhamishwa . Maafisa wa usalama huko Nandi wamethibitisha kwamba Ngeiywo alitakiwa kufika Jumba la Vigilance wiki jana kufuatia tukio hilo ambalo baadaye lilisababisha gavana Sang kukamatwa na maafisa wa DCI na kufikishwa mahakamani Kisumu .