Msanii huyo wa Tanzania amekuwa katika uhusiano na wanawake wengi lakini hakuna aliyewahii kuuteka moyo wake ili kustahili kuchorwa kwa vyovyote katika mwili wake, lakini Diamond sasa amedhihirisha jinsi anavyomuenzi mama Dangote .
Amekuwa na tattoo hiyo kwa miaka mitatu sasa na hivi karibuni Mamake walionyesha picha za tattoo hizo na kuandika ;
CHAKUDEKA MTOTO WA MAMA ALHAMDULILLAAH ASANTE KWA ZAWADI HII @DIAMONDPLATNUMZ
Diamond ana michoro mingine kadhaa ya tattoo katika mwili wake na moja katika kifua chake inasoma ;
I BELIEVE IN GOD.
Katika mkono wake wa kushoto ameweka herufi N,T,N na D ambayo ni majina ya watoto wake; Nillan, Tiffah, Naseeb, na Dylan.
Pia ana michoro ya tatto ya tarehe mbili spesheli kwake moja ni siku yake ya kuzaliwa 2-10-1989 na nyingine iliyoandikwa kwa kiroman ni siku ya kuzaliwa kwa mamake; 7-7-1967.