Mbwa alaumiwa kwa kumnyima Mkenya ushindi katika marathon

Mwanariadha Robert Kimutai Ng’eno alifukuzwa na mbwa wakati wa mashindano ya riadhaa ya Buenos Aires wiki iliyopita.

Muhtasari

•Mwanariadha huyo alionekana akiongoza huku amesalia na kilomita 4 kukamilisha mbio hizo, wakati mbwa alipojitokeza na kuanza kumfukuza

•.Raia wenzake wa Kenya Cornelius Kiplagat na Paul Kipngetich Tanui waliibuka katika nafasi ya kwanza na ya pili mtawalia.

Robert Kimutai Ng'eno alikuwa akiongoza mbio hizo mbwa alipotokea
Robert Kimutai Ng'eno alikuwa akiongoza mbio hizo mbwa alipotokea
Image: BBC

Seneta mmoja nchini Kenya amekosoa mashirika ya michezo ya kushindwa kuchukua hatua baada ya mbwa kumfukuza mwanariadha Robert Kimutai Ng’eno wakati wa mashindano ya riadhaa ya Buenos Aires wiki iliyopita.

Ripoti zinasema mwanariadha huyo alionekana akiongoza akiwa amesalia na kilomita 4 kukamilisha mbio hizo, wakati mbwa alipojitokeza na kuanza kumfukuza.

Licha ya juhudi za baadhi ya watazamaji kumfukuza mbwa huyo, tukio hilo lilionekana kumfanya Ng’eno kupoteza mweleko na hatimaye kumalizia katika nafasi ya tatu kwenye mbio hizo.

Raia wenzake wa Kenya Cornelius Kiplagat na Paul Kipngetich Tanui waliibuka katika nafasi ya kwanza na ya pili mtawalia.

Picha inayoonyesha mbwa akimfukuza Ng’eno imesambaa sana katika mitandao ya kijamii na baadhi wameuliza kwanini juhudi zaidi hazikuchukuliwa kumlinda wanariadha.

“Mwanariadha hakupewa heshima yake na kukabiliwa na kejeli,” alisema Seneta Samson Cherargei kwenye mtandao wa X (zamani uliokuwa ukijulikana kama Twitter).

Alisema kwamba Waziri wa Michezo wa Kenya Ababu Namwamba na shirika la wanariadha la Kenya hawakusimama na mwanariadha huyo, huku akiongeza kwamba “hawajachukua hatua kwa kueleza malalmishi yao au kutoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi na mamlaka za Argetina.