logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kevin De Bruyne asema yuko tayari kwa uwezekano wa kuhamia ligi ya Saudi

De Bruyne amefunguka kuhusu uwezekano wa kuhamia Saudi huku akisalia na mkataba wa mwaka moja

image
na Radio Jambo

Football04 June 2024 - 12:19

Muhtasari


•Kevin De Bruyne amefunguka kuhusu kuhamia ligi ya Saudi iwapo ofa yoyote itatokea.

•Mchezaji huyo amedai kuwa cha msingi kwake ni pesa hasa ikizingatiwa kuwa miaka yake imeenda na maisha yake ya baadaye ni ya muhimu mno.

Kevin De Bruyne amefunguka kuhusu uwezekano wa kuhamia ligi ya Saudi iwapo ofa yoyote itatokea hivi karibuni ama mwishoni mwa kandarasi yake.

Kiungo wa kati wa Manchester City Kevin De Bruyne amesema kuwa yupo tayari kuhamia kwenye ligi ya Saudi iwapo ofa yoyote itatokea.Kwenye mahojiano na jarida la Hlsport,De Bruyne amedokeza kuwa katika umri wake lazima mtu awe na uwazi na awe na maoni ya baadaye hasa kama mchezaji ambaye miaka imeenda.

"Unazungumza juu ya pesa nyingi sana katika kile ambacho kinaweza kuwa mwisho wa kazi yangu.Wakati mwingine unapaswa kufikiria kuhusu hilo.Nikicheza huko kwa miaka miwili,nitaweza kupata kiasi cha ajabu..' De Bruyne alisema.

Mchezaji huyo aidha amefichua kuwa amekuwa akicheza mpira kwa zaidi ya miaka 15 na huenda akijumulisha kiwango cha fedha alichopokea kwa hizo miaka kisifikie kile cha Saudi kwa miaka miwili.

"Kabla ya hapo nililazimika kucheza  mpira wa miguu kwa miaka 15.Huenda hata nisifikie kiasi hicho..unafaa kufikiria ni nini kinachowezakumaanisha baadaye..."

 

Kwa sasa De Bruyne amesalia na mkataba wa mwaka mmoja,Manchester City.Mchezaji huyo amecheza mechi 382 kwa miaka tisa tangu ajiunge na Manchester City,huku akishinda mataji sita ya ligi kuu ya Primia na kombe la klabu bingwa Ulaya.

Ligi kuu ya Saudi ilianza  kupata umaarufu baada ya Christiano Ronaldo kujiunga na Al-Nassr mwaka  wa 2023. Wachezaji wengi wababe wamejiunga na vilabu vya Saudi kama vile  Karim Benzema,Ngolo Kante,Fabinho,Jota,Neymar na wengineo.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved