Mbunge wa Embakasi mashariki Babu Owino amezungumza kuhusu gharama ya inayoongezeka ya kumtibu Felix Orinda au DJ Evolve ambayo sasa imefikia shilingi milioni 7 katika Nairobi Hospital .
Mbunge huyo ndiye aliyempiga risasi DJ Evolve katika eneo la burudani la B Club mwezi januari na aliahidi kwamba atagharamia matibabu yake . Babu amesema familia ya DJ huyo haifai kuwa na wasi wasi kuhusu bili
Pia amekanusha ripoti kwamba alikwepa kulipa gharama zaidi za matibabu baada ya kutoa malipo ya mwanzo ya shilingi laki sita akiongeza kwamba kufikia sasa amelipa shilingi milioni tano .