‘Msijali kuhusu Bill’ ,Babu Owino aiambia familia ya DJ Evolve  

Mbunge wa  Embakasi mashariki Babu Owino  amezungumza kuhusu  gharama ya inayoongezeka ya kumtibu  Felix Orinda au DJ Evolve  ambayo sasa imefikia shilingi milioni 7 katika Nairobi Hospital .

Mbunge huyo ndiye aliyempiga risasi DJ Evolve  katika eneo la burudani la B Club mwezi januari  na aliahidi kwamba atagharamia matibabu yake . Babu amesema familia ya  DJ  huyo haifai kuwa na wasi wasi kuhusu bili

Pia amekanusha ripoti kwamba  alikwepa kulipa gharama zaidi za matibabu baada ya kutoa malipo ya mwanzo ya shilingi laki sita  akiongeza kwamba kufikia sasa amelipa shilingi milioni tano .