Nderitu amekataa kuongeza muda huo wa miaka mitano akingoja marekebisho yua ombi la chama hivho kutaka muda wa Mudavadi kama kiongozi wa ANC kuzidishwa hadi baada ya janga la Covid 19 .
Katiba ya ANC maafisa wa chama watachaguliwa kuhudumu kwa miaka mitano ambapo baada ya muda huo uchaguzi utaandaliwa na maafisa wapya kuchaguliwa .
Mnamo juni tarehe 26 ANC iliamua kupitia mkuano maalum wa baraza la usimamizi kwamba wale ambao muda wao kuhudumu umekamilika wataendelea kushikilia nafasi hizo hadi baada ya janga la corona .
Hatamu ya washikilizi wa nafasi hizo akiwemo Mudavadi ilitamatika Juni tarehe 15
Katika jaribio la kufuata katiba yake chama hicho kilisongesha mbele uchaguzi wake hadi baada ya janga na corona .Iliwasilisha ombi hilo kwa msajili wa vyama Anne Nderitu .
Siku ya Jumanne Nderitu ameliambia gazeti la The Star kwamba afisi yake imekataa ombi hilo la ANC kuzidisha muda wa washikilizi wa nafasi za uongozi kwani pendekezo hilo linazuiwa na mianya na ukiukaji wa sheria inayosimamia vyama vya kisiasa
“ Kuna mianya na msajili wa vyama amekishauri chama cha ANC kurekebisha na kuziba mianya hiyo kwanza ili kuafikiana na mahitajiya sheria ya vyama vya kisiasa’ amesema Nderitu kupitia simu