Wahu na Nameless pia sio watu wa kuigiza kuhusu maisha kwani wao husema ukweli kuhusu ugumu na changamoto za ndoa bila kuficha au kupaka rangi mambo katika maisha yao. Wahu ambaye ni mama ya wasichana wawili warembo, maajuzi amezungumza kuhusu kupata mtoto mwingine. Katika mahojiano na Word Is, msanii huyo mwenye umri wa miaka 40 amesema amefunga uzazi.
Namless na Wahu wamekuwa pamoja kwa miaka 15 na yaonekana washafanya uamuzi wa kufunga sura ya uzazi kwani Wahu ana lalama zake akisema;
“ Nazidi kunenepa tu , sifikiri nataka mtoto mwingine. Mtoto huchukua miaka yako mitatu kabla aweze kujifanyia lolote …’
“ Niko sawa. Kifunga mimba wangu Nyakio anakaribia kutimu umri wa miaka saba na nafurahia kwamba anajifanyia vitu vingi mwenyewe; anaoga na kula pekee yake …’
Msanii huyo wa gospel anasema anafahamu kwamba baraka huja kupitia watoto lakini ameridhika na wawili hao. ‘ Ni raha lakini mimi nimeridhika na wasichana wangu wawili.’ Wahu anasema.
Msimamo wake hata hivyo unakinzana na wa mume wake Nameles ambaye miaka michahe iliyopita alifichua matamanio yake ya kupata mtoto mwingine mvulana... Hadi sasa vitakuwa vita vya panzi na huenda Nameless akisinzia basi mkewe Wahu atakuwa na usemi wa mwisho na kufunga kabisa fursa ya yeye kuwa baba ya ‘ndume’.