Picha za Rayvanny na mrembo Nana zinazomkosesha usingizi Fayhma

Rayvanny_Nana_mpasho7__1575275289_51088
Rayvanny_Nana_mpasho7__1575275289_51088
Hatimaye Nana anayehusishwa na kuvunja penzi moto la Rayvanny na Fahyma amefunguka kuhusu kisa hicho.

Katika mahojiano na kituo cha habari nchini Tanzania, Fayma amekana habari za kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na staa huyu.

Mrembo huyu amesema kuwa tukio la kutemana kwa wanandoa hawa ni kitu na ambacho kilimvunja moyo sana.

"Niliskia kuwa Fahyma( Mke wa Rayvanny) alikuwa amechapisha posti kunihusu. Mimi nilikuwa nafanya kazi yangu ila sio mambo mengine. Nimekuwa naumwa sana na kichwa kutoka tukio hilo lifanyike..." Alisema Nana.

Haya yanajiri huku staa wa mkwaju wa Tetema, Rayvanny akifunguka A-Z kuhusu kutemana na mkewe Fahy Vanny.

“Sina ufahamu wa kiki. Naishi maisha yangu. Nikidondosha ngoma mashabiki zangu huipokea freshi. Ulichokiona ndicho…” Alisema Rayvanny.

“Sipo kwenye mahusiano na Nana, tena ana mahusiano yake ambayo nayaheshimu sana sana.Kichupa ni kizuri kwani kinaonyesha ukweli na mapenzi yapo. Nilitaka video hiyo iwe jinsi ilivyo..” Rayvanny aliongeza.

Rayvanny na Nana walikana kabisa kuwa katika mapenzi ya kisirisiri.

"Tulipiga picha nyingi na hiyo ilikuwa sehemu ya kazi yangu. Mimi na Rayvanny ni marafiki. Hatuna mahusiano ya kimapenzi. Nipo kwenye uhusiano na mwanamume wangu na kila mtu anajua. Siwezi kufanya kufanya vituko vya kijinga hivi kwa sababu tumekuwa naye kwa miaka minne." Alisema Nana.

Tazama picha za Rayvanny na Nana: