Raila akutana na Robert Njura jamaa aliyemvusha kwa boti hadi Uganda mafichoni

Aliyekuwa waziri mKuu Raila Odinga amekutana na    Robert Njura ambaye aliokoa maisha yake mwaka wa 1991 alipokuwa akikimbia kwenda mafichoni nchini Norway akitoroka utawala wa rais Daniel Moi .

Njura aliyekuwa kijana wa maka 19 wakati huo alimvusha Raila katika ziwa Victoria kuingia nchini Uganda  wakati Bwana Odinga alipokuwa akisakwa na maafisa wa polisi . Njura wakati huo alikuwa mwanafunzi wa kidato cha tatu na kwa kazi yake ya kumvusha Odinga hakujua  mteja wake alikuwa nani na baada ya kulipwa shilingi 2000 kwa kazi yake ndipo alpojulishwa kuhusu ‘mteja’ aliyevushwa kuingia Uganda .

Kulingana naye ,baadhi ya vijana katika eneo hilo walikataa kumvusha bwana Odinga kwenda Uganda kutumia boti lakini yeye alijitolea . Odinga amesema mchango wa  Njura  katika kubadilisha mkondo wa siasa nchini kupitia hatua hiyo yake ni mkubwa na hauwezi kusahaulika .

Odinga  ameandika ujumbe katika mitandao  ya kijamii akimsifu Njura kwa hatua hiyo yake akisema ;

‘ Ni  heshima kubwa kukutana  na Robert Njura aliyenivisha kwa boti nchini Uganda nikienda mafichoni Norway .Njura ni dhihirisho kwamba ukakamavu ,kujitolea  na nguvu za vijana kunaweza kuafikia mengi. Mungu ambariki pamoja na vijana wetu katika maadhimisho haya yam waka wa kumi  tangu tuipate katiba mpya’ Odinga ameandika