Siku chache baada ya kutuzwa, mkewe Mbusii asherehekea siku ya kuzaliwa

mama stacy
mama stacy
Kwa takriban wiki moja hivi, nyumba yake mtangazaji Daniel Githinji Mwangi, almaarufu, 'Mbusii' imejawa na furaha na mihemko tele. Hii ni kufuatia kutuzwa kwake Mbusii kama mtangazaji bora bara la Africa huko Ghana.

Tuzo hizo huwatambua vijana Afrika nzima kuanzia miaka 18 hadi 35 na Mbusii ndiye aliyepokea tuzo la muafrika bora katika nyanja ya utangazaji aidha redioni au TV.

Kabla hata ya vumbi hilo la ushindi kutulia, familia hiyo hii leo inasherehekea siku ya kuzaliwa kwa mkewe Mbusii, anayetambulika na wengi kama 'Mama Stacy'.

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Insta, Mbusii alichukua nafasi hiyo asubuhi na mapema na kumtakia mpenziwe na mama wa wanao siku yenye fanaka na baraka tele.

Mbusii alichapisha picha ya wawili hao na ujumbe ufuatao;

Happy birthday Mkondi Wa Mbusii.... More blessings to you, more life, for life

https://www.instagram.com/p/B5oclZuJUGZ/

Mashabiki wa Mbusii nao hawakuwachwa nyuma;

John: Happy birthday

Cliff dogo: HBD mrs HSC

Ken logic: Jah bless