McCarter amekuwa akitumia mitandao ya kijamii na hasa Twitter kukashifu viongozi wanaohusika na wovu wa kupora mali ya umma bila kujali mustakabali wa wakenya . Hata hiyo miongoni mwa jumbe zake hizo la kulaani ufisadi ,ujumbe aliotuma katika Twitter kwa lugha ya Kiswahili umepokelewa kwa hisia tofauti huku baadhi ya watumizi wa twitter wakimkejeli kwa kuvuruga ngeli na matumzi ya maneno ya Kiswahili lakini wengi wakimsifu wa ukakamavu wake kujaribu kuwasilisha ujumbe wake kwa lugha ya Kiswahili inayofahamika na wengi nchini .
Balozi McCarter sio mgeni kwa lugha ya Kiswahili kwani anaweza kuzungumza Kiswahili hata kuwaliko baadhi ya wakenya .Pia amechukulia ukosiaji dhidi yake kwa njia ya kistaarabu kwa kuahidi kujifunza zaidi .