Magavana wameonya kwamba mfumo huo wa utawala huenda hautastahimili mgogoro wa ukosefu wa fedha iwapo hakuna kitakachofanywa kwa haraka kubadilisha hali hiyo .
Hazina ya kitaifa bado haijatoa shilingi bilioni 32 zinzofaa kusamabzawa kwa kaunti kwa mwaka wa kifedha wa 2019-20.
Waziri wa fedha Ukur Yattani hajatoa ratiba ya ni lin pesa hizo zitatolewa .
Kibaya zaidi ni kwamba kwa sasa kuna utata katika senate kuhusu mfumo unaofaa kutumiwa kugawa pesa kwa serikali za kaunti .
Kaunti nyingi hazina fedha na zimekuwa zikitumiwa shilingi bilioni 5 za kushughulikia janga la Covid kuendesha oparesheni nyingine .
Kaunti haziwezi kugawana shilingi bilioni 316.5 zilizotengwa kwa mwaka wa kifedha wa 2020/2021 bila mfumo huo kuafikiwa .kucheleweshwa kwa mwafaka huo huenda kukazua matatizo zaidi kwa magavana .