Uhuru aliwasil katika uwanja wa Nyayo saa sita kasorobo kabla ya kufungua uwanja huo .
Rais aliandamana na waziri wa Spoti Amina Mohammed ,gavana wa Nairobi Mike Sonko na maafisa wengine wa serikali .
Uhuru alitembea katika uwanja huo akionyesha mageuzi yaliyotekelezwa katika ukarabati .
Uwanja wa Nyayo ulifungwa mwaka wa 2018 kwa ukarabati ili kuandaa mashindano aya Chan mwaka wa 2018 lakini mashindano hayo yakahamishwa hadi Morocco .
Rais Uhuru Kenyatta aliiagiza wizara ya spoti kuweka mikakati ya kuzuia utimizi wa dawa zilizoharamishwa miongoni mwa wanaspoti .
" Tumekuwa na visa vya wanaspoti wetu kutumia dawa zilizoharamishwa ingawaje visa hivyo ni vichache ,vinahofisha’ amesema rais
" Toeni raslimali za kuzuia utumizi wa dawa hizo kwa kuzidisha uhamasisho ,vipimo na kuripoti’
Akizungumza katika uwanja wa Nyayo rais amesema sifa za Kenya katika michezo zimejengwa kwa msingi wa kushiriki mashindano kwa njia ya kweli .
Uhuru amesema kufikia mwaka ujao maafisa wa KDF watakuwa na uwanja wao katika eneo la Langata