Mwanajinakolojia Allan Ikol anasema kuvalia chupi za kubana ni jambo linaloathiri kiwango cha mbegu zako za kiume na hata ubora wake.
Ikol anasema uzalishaji wa mbegu huregemea kiwango fulani cha joto na sehemu iliyojibana huwa na joto jingi. Joto hilo ndilo linaloathiri uzalishaji wa mbegu za kiume. Anaongeza kwamba wengi hufanya kosa la kulala usiku wakiwa na nguo za ndani zinazowabana sana bila kufahamu madhara yake.
Pia kuna hili tatizo la wanaume kuwa na tabia ya kuvalia chupi moja zaidi ya mara moja . wengi hufikiri hatua hiyo haina madhara lakini Dkt .Ikol anasema ,unajitia katika hatari ya kupata maambukizi katika sehemu zako za uume endapo utarejelea chupi yako kila mara .Anasema harufu ,msuguo wa ngozi na jasho ni mchanganyiko unaoweza kusababisha ukuaji bakteria hatari inayoweza kukudhuru .
Ikol anasema sio ajabu kumwona mwanamme aliyejikwatua kwa suti nadhifu sana lakini ndani ,Chupi ina matundu kama kichungi !
Je, ni kweli kwamba wanaume hawatalii maanani usafi wa chupi zao?