•Mchekeshaji Eric Omondi alionyesha Mpenzi wake kwenye ukurasa wake instagram huku akimtakia siku njema ya wapendanao.
Mchekeshaji Eric Omondi alitambulisha mpenzi wake siku ya Jumatatu kupitia ukurasa wake instagram huku akimtakia siku njema ya wapendanao.
Wanamitandao walichwa vinywa achama kwani sio wengi waliotarajia mcheshi huyo kupiga hatua kama ile.
Omondi alionekana pamoja na mwanadada anayetambulika kama Lyne wakiwa wamevaa mavazi mekundu.
Kama ilivyokawaida siku ya wapendanao kupostiana na kuandikiana maneno yenye hisia za mapenzi, Mcheshi huyo hakusazwa nyuma ambapo alichukua nafsi hiyo kumwonyesha mwanadada huyo mahaba.
Ikumbukwe ni hivi majuzi Mcheshi huyo alindokeza kwamba alimpatia Lyne gari lake na hana haraka ya kulichukua.
Mcheshi huyo alikuwa miongoni mwa wanaume waliohudhuria Men Conference siku ya Jumatatu lakini alichukua fursa hiyo ya kipekee kuonyesha ulimwengu kuwa ana kipenzi cha roho yake.
Wengi wanamjua Eric Omondi kama mchekeshaji mwenye vituko na sarakasi ambazo humsaidia kutengeneza kiki lakini tokea hili ni kweli mapenzi ni kikohozi hayafichika.