•Rapa kutoka Marekani Kanye West amepiga kalamu wakili aliyekuwa akisimamia kesi yake ya talaka na mkewe Kim Kardarshian.
Rapa kutoka Marekani Kanye West amepiga kalamu wakili aliyekuwa akisimamia kesi yake ya talaka na mkewe Kim Kardarshian.
Kanye amekuwa na malumbano ya nyumbani na aliyekuwa mke wake, Kim Kardashian ambaye aliwasilisha ombi la kutaka kutalikiana naye.
Kulingana na mtandao wa TMZ, Kanye hawajakuwa na uhusiano mwema na wakili Chris Melcher ikibainika kuwa mawasiliano yao yamekuwa chache siku za hivi karibuni.
Inasemakana kuwa kuna wakati Kanye alikuwa anadai kusuluhisha suala hilo nje ya mahakama.
Rapa huyo ameajiri wakili Samantha Spector,ambaye hivi majuzi alimwakilisha Nicole Young katika talaka yake na Dk. Dre.
Kesi ya Kanye imeratibiwa siku ya Jumatatu ijayo, ambapo jaji anatarajiwa kutoa uamuzi wa talaka yao na Kim rasmi.
Aidha Kim aliwasisilisha ombi mahakamani la kutaka kutumia video kuwasilisha malalamishi yake na sababu za kuomba talaka.