Elon Musk amtupia dongo mfanyibiashara aliyeondoa tangazo lake kwenye X

mfanyibiashara huyo wa migahawa aliondoa matangazo yake X kufuatia wasiwasi wa mtandao huo kutumika kueneza chuki dhidi ya Wayahudi.

Muhtasari

• Musk akijibu hatua hiyo alisema kwamba tangazo lenyewe hata halikuwa la kushawishi.

• hapo, Hilton amehamishia matangazo yake kwenye TikTok na Instagram.

Elon Musk na Paris Hilton
Elon Musk na Paris Hilton
Image: X

Elon Musk Jumapili alimdhihaki mwanahabari na mfanyibiashara wa Marekani, Paris Hilton na kampuni yake ya Be an Icon cookware baada ya mrithi wa hoteli hiyo kuondoa utangazaji wa kampuni yake kwenye jukwaa lake la X, awali likijulikana kama X.

Inaarifiwa kwamba Hilton alifikia uamuzi wa kukatisha biashara ya kulipia matangazo ya upishi wake kwenye X kutokana na wasiwasi kuhusu maudhui ya chuki dhidi ya Wayahudi yanayochapishwa kwenye mtandao wa kijamii.

'Tangazo lenyewe hata halikuwa la kushawishi kusema tu ukweli,” Musk aliandika kwenye moja ya tweet katika mtandao huo. “Sidhani Paris hupika sana.”

Tweet ya mzaliwa huyo wa Pretoria, Afrika Kusini ilikuja kumjibu mtumiaji ambaye alichapisha picha ya 2005 ya Hilton, 42, akionekana kama mwanamitindo kwenye onyesho la mitindo lililowekwa na dadake Nicky huko Las Vegas, akiwa amevalia blausi iliyodaiwa kusomeka 'Stop Kuwa Maskini.'

Kulingana na gazeti la New York Post, kampuni ya Hilton ilikuwa moja katika kundi lililochota dola zao za utangazaji kutoka kwa kampuni ya Musk baada ya Musk mnamo Novemba 15 kuidhinisha tweet iliyokuwa na nyara za anti-Semitic, kuwanyanyapaa Wayahudi.

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa X Linda Yaccarino mnamo Oktoba alisema kuwa kampuni ya Hilton 11:11 Media ilikuwa imeweka wino kwenye mpango wa tangazo la kugawana mapato kwenye jukwaa la mitandao ya kijamii.

Hilton alisema wakati huo: 'Pamoja, tutakuwa tukigundua njia mpya za kuwasiliana nanyi nyote kwenye video, video za moja kwa moja, ununuzi wa moja kwa moja na hata Spaces. Na ndio tunaanza. Mtapenda.'

Baada ya kuamua kuondoa tangazo lake X, Hilton, ambaye alikuwa na kipindi cha Netflix kinachoitwa Cook with Paris, tangu wakati huo amehamishia matangazo yake ya upishi kwenye Instagram na TikTok.