Tabitha Karanja ataka mahakama kumshtaki upya Omar Lali kuhusiana na kifo cha binti yake Tecra

Muhtasari

 

  •  Tabitha Karanja anataka Lali kufunguliwa upya mashtaka 
  •  Lali na Tecra walikuwa katika uhusiano kwa miezi 10 kabla ya kifo chake 
  • Familia ya Tabitha inataka kesi kufanywa Nairobi 

 

Tecra 3
Lali na marehemu Tecra Muigai Tecra 3

Familia ya Tecra Muigai inamtaka mkurigenzi wa mashtaka ya umma kumshtaki upya  aliyekuwa mpenzi wake Lali Omar kwa mauaji yake .

Tecra  aliaga dunia mei tarehe 2 katika NAIROBI Hospital  baada ya kusafirishwa kutoka Lamu baada ya kudaiwa kuanguka  akiwa hotelini .Alikuwa na umri wa miaka 29 .

Lali, mwenye umri wa miaka 52 alishtakiwa kwa  mauaji ya Mpenzi wake  julai tarehe 13 lakini alikana mashtaka hayo .

 

 Hata hivyo mkurugenzi wa mashtaka ya umma  aliondoa mashtaka dhidi ya Omar  na kuagiza uchunguzi ufanywe kuhusu kifo cha Tecra .

 Katika tukio jipya sasa mamake Tecra,Tabitha Karanja  amewasilisha kesi kortini akisema familia yake ilishangazwa na uamuzi wa DPP .

Karanja  anamtaka DPP kuwashurutisha wachunguzi kuziba mianya katika faili ta Lali ili aweze kujibu mashtaka ya mauaji ya Tecra .

 Pia amesema familia yake inataka kesi hiyo kusikizwa Nairobi ambako binti yao  aliaga dunia  .Amesema wahusika wote katika kesi hiyo ,familia ,wachunguzi na wataalam wengine wanaohitajika wanaishi  Nairobi .

Karanja  amesema familia yake inahofia usalama wao huko Lamu ambako Lali anajulikana nawatu wengi wakiwemo wahudumu wa boti .

 Amemshtumu DPP kwa  kutapatapa na kesi hiyo huku ikimshtumu kwa kuwa kikwazo kwa familia hiyo kupata haki .

  Wachunguzi kutoka DCI wanaochunguza kifo cha Tecra wamesema Lali alikuwa mpenzi mwenye wivu na wakati mwingine alipigana na rafiki zake na watu waliodaiwa kuwa mahasimu wake. Ripoti yao imesema Tecra alikuwa mateka wa mapenzi ya Lali  na alikuwa amefanya kila jitihada kujinasua  .Uhusiano wao ulikuwa umedumu miezi kumi kabla ya kifo chake