Uhuru akutana na viongozi wa Kisii Ikulu na kujadili maendeleo

Muhtasari
  •  Sherehe za mwaka huu za Mashujaa zitaandaliwa Kisii
  • Rais aliwashukuru viongozi wa Kisii kwa kukubali kuwa wenyeji wa sherehe za Mashujaa
  • Waziri Matiang'i alikariri kujitolea kwa serikali kukamilisha miradi ya maendeleo katika eneo hilo 

 

Rais Uhuru Kenyatta akikutana na viongozi kutoka Kisii

 

 Rais Uhuru Kenyatta amefanya mkutano na viongozi  kutoka Kisii  ambapo amejadili masuala ya maendeleo ya eneo hilo . Sherehe za mwaka huu za siku ya mashujaa pia zitafanyika Kisii .

 Sherehe hizo zitaandaliwa katika uwanja wa Kisii  na mkutano huo ulimpa rais kenyatta fursa ya kukadiria miradi ya maendeleo  pamoja na viongozi wa eneo hilo .

 Wakiongozwa na magavana  James Ongwae wa Kisii na  John Nyangarama wa Nyamira  viongozi hao walizungumza na rais Kuhusu  miradi mbali mbali ya barabara ,elimu na soko kwa mazo ya watu wao .

 Katika waraka maalum uliowasilishwa kwa rais na gavana Ongwae  viongozi hao akiwemo mwenyekiti wa muungano wa watalaam kutoka Kisii  John Simba  na mwenyekiti  baraza la wazee wa jamii hiyo  James Matundura  ,walimshukuru rais  kwa mipango kadhaa ya amendeleo inayoendeshwa na serikali kuu .

 Walizitaja barabara kadhaa ,miradi ya maji  ,hospitali na masoko ya daraja mbili na Nyakoe kama baadhi ya miradi  inayosaidia kuboresha hali ya aisha ya wakaazi .

 Wakati huo huo viongozi hao walimtaka rais kuhakikisha kwamba miradi inayoendeshwa kwa sasa inatamatishwa kwa wakati .  Rais alikuwa na mawaziri   Fred Matiangi wa usalama wa ndani , James Macharia wa uchukuzi na Mutahi Kagwe wa Afya wakati wa mkutano huo .