- Tukio lilitokea mwaka jana wakati Jumwa alipovamia mkutano wa ODM
- Mwanamme mmoja alipigwa risasi katika patashika iliyozuka
Mkurugenzi wa mashtaka ya umma Noordin Haji ameidhinisha kushtakiwa kwa mbunge wa Malindi Aisha Jumwa kwa mauaji ya mwanamme mmoja wakati wa ghasia zilizozuka kwenye uchaguzi mdogo wa wadi ya Ganda mwaka uliopita .
Mwanamme huyo alipigwa risasi wakati wa patashika iliyozuka huko Malindi oktoba mwaka jana wakati wafuasi wa Jumwa aaliposhambuliana na wafuasi wa chama cha ODM
Kisa hicho kilifanyika wakati Jumwa alipovamia mkutano wa ODM akitaka kujua kilichokuwa kikifanyika wakati huo wa usiku baada ya muda wa kampeini kutamatika . Maafisa wa ODM walisisitiza kwamba mkutano huo ulikuwa wa mafunzo kwa maajenti wa chama cha ODM .
Jumwa anatarajiwa kufanyiwa ukaguzi wa kiakili wiki ijayo kabla ya kufikishwa kortini kujibu mashtaka . Mwanamme aliyeua katika tukio hilo alikuwa jamaa ya mgombeaji wa ODM Katika uchaguzi huo mdogo Reuben Katana ambaye aliibuka mshindi