Pingamizi

William Ruto: Haya ndio mambo ninayotofautiana nayo katika BBI

Ruto asimama kidete dhidi ya baadhi ya mapendekezo ya BBI

Muhtasari

 

  • Amesema  katiba ya 2010 iliwapa polisi kuhudumu bila muingilio wowote wa  kisiasa  .
  • Amesema katika mapendekezo ya BBI senate imepunguziwa nguvu za kuamua kuhusu raslima za kaunti na matumizi yake
  • Timu haziwezi kumchagua refarii -Ruto

 

Naibu Wa rais William Ruto siku ya jumatatu ameeleza pingamzi yake kuhusu baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti ya BBI  jinsi ilivyo sasa akisema mambo hayo yanafaa kurekebishwa  na wakenya wote kupewa fursa ya kutoa michango yao ili kuiboresha hata Zaidi .

 Idara ya mahakama

 Ruto amesema   kwamba pendekezo la kuundwa kwa afisi ya  kutoa malalamishi kuhusu idara ya mahakama ambayo mshikilizi wake atateuliwa na rais ni jambo am,balo litavuruga uhuru wa idara hiyo .  Ruto amesema hiyo inaweza kulirejesha taifa katika siku za kale ambapo  maamuzi ya majaji yaliamuliwa na rais kupitia simu .

 Amesema wakenya wengi pia wanalazimika kusafiri mbali kupata huduma za mahakama na idara hiyo inafaa kupewa ufadhili wa kutosha .

" Tunafaa kuanza kuitumia hazina yay a idara ya mahakama ili iweze kuwaajiri majaji zaidi na kujenga korti katika kila sehemu za nchi kuwahudumia wakeny’ amesema Ruto .

Naibu wa Rais William Ruto

 Tume ya uchaguzi

 Kuhusu pendekezo la  makamishna wa uchaguzi kuteuliwa na vyama vya kisiasa Ruto amesema hatua hiyo ni kama kuzipa baadhi ya timu maamlaka ya kumteua refarii katika michuano

 “ swali ambalo najiuliza ni je  mchuano kama huo kutakuwa na haki ?’

 Kuhusu kuzuia mshindi katika uchaguzi kuchukua yote Ruto alishangaa jinsi mapendekezo hayo yatakavyozuia hilo ilhali rais ,naibu wake na waziri mkuu na manaibu wake watakuwa kutoka upande mmoja wa kisiasa .

 Huduma ya polisi

Ruto, alizungumza kuhusu huduma  ya polisi na kuundwa kwa  baraza la polisi .amesema  katiba ya 2010 iliwapa polisi kuhudumu bila muingilio wowote wa  kisiasa  .

 

‘Pendekezo la kuwa na baraza la polisi litakaloonozwa na waziri ni kuvuruga uhuru wa polisi’

 Ugatuzi

 Kuhusu  kuongezwa kwa mgao wa fedha za  kauti kutoka asilimia 15 hai 35 Ruto amesema hilo linafaa kuambatana na bunge la senate lenye nguvu . Amesema katika mapendekezo ya BBI senate imepunguziwa nguvu za kuamua kuhusu raslima za kaunti na matumizi yake . Pia amepinga kuondolewa kwa nafasi ya mwakilishi wa akina mama kutoka bunge . Amesema pia kwamba suala la uundaji wa nafasi za ajira na kuboresha biashara ndogo ndoo na za kadri ni jambo linalofaa kutathminiwa upya

 Hotuba ya Ruto kuhusu masuala hayo ya BBI  haikuwapendeza baadhi ya wajumbe katika ukumbi wa Bomas lakini naibu wa rais alisema ana haki ya kuhoji na kuyazua katika mjadala kuhusu njia za kuboresha ripoti hiyo .Baadhi ya wajumbe walianza kumkemea Ruto kwa kelele na akatamatisha hotuba yake kwa kumualika rais Uhuru Kenyatta ambaye alionekana kuiunga mkono ripoti hiyo jinsi ilivyo akisema masuala mengine yanayoonekana kama udhaifu wa ripoti hyo yanaweza kushughulikia mchakato mzima ukiendelea .