- Agnes Wangui anataka vipimo vya DNA kufanywa ili kuthibitisha kwamba baba ya watoto wake ni Mbunge Murunga
- Anataka kuhusishwa katika mipango ya mazishi ya mbunge huyo wa zamani wa Matungu
- Amesema alianza uhusiano na marehemu mwaka wa 2013
Mwanamke anayedai kwamba ni mpenzi wa marehemu mbunge wa Matungu Justus Murunga amewasilisha kesi kortini ili kuzuia kuzikwa kwa mbunge huyo .
Kupitia wakili wake Danstan Omari ,Agnes Wangui wanawtaak wajane wawili wa Murunga - Christabel na Grace na hifadhi ya maiti ya Lee wazuiwe dhidi ya kumzika mbunge huyo .
Pia anataka mahakama kutoa ruhusa ya kuchukuliwa kwa sampuli za DNA za mbunge huyo na watoto wa Agnes ili kuthibitisha kwamba watoto hao ni wa Murunga .
Pia anataka mwili wa mbunge huyo kuhifadhiwa Lee hadi wakati sampuli ya DNA itakapotolewa pakiwepo mwanapatholojia aliye na leseni ambaye atateuliwa na pande zote mbili .
Agnes, amesema watoto wake wawili ni wa marehemu mbunge huyo . Amesema anahofia wajane wake wawili wanaweza kupanga njama ya kumfungia nje pamoja na wanawake katika mipango ya kumzika Murunga .
Kupitia waraka kwa mahakama amesema amemjua mbunge huyo kwa mika saba tangu mwaka wa 2013 alipokuwa msimamizi katika shamba la Embakasi na yeye alipokuwa mfanyibiashara katika eneo la Ruai .
Agnes amesema baada ya kuanza kwa uhusiano wao wa kimapenzi na kuwapata watoto wawili ,Murunga alimkodishia nyumba katika mta wa Ruai.Uhusiano wao ulianza kuvurugika mwaka wa 2017 baada ya mbunge huyo kushinda kiti cha ubunge cha Matungu