Afisa mkuu mtendaji wa hospitali ya Mama Lucy na watu wengine wawili ambao wanashtumiwa kwa sakata ya uuzaji wa watoto watasalia rumande kwa siku ili kuruhusu uchunguzi dhidi yao kufanyika .
Afia huyo mkuu Emma Mutio na Makallah Fred na Regina Musembi waliwekwa rumande baada ya agizo la hakimu Bernad Ochoi .
Katika uamuzi wake Ochoi amesema maafisa wa uchunguzi wako sawa kuwa na hofu kuhusu uwezekano wa washukiwa kuvuruga ushahidi wa stakabadhi dhidi yao
Makallah alifichuliwa katika uchunguzi uliofanywa na BBC alipokuwa akijadiliana na mwanahabari wa BBC kuhusu mpango wa kumuuza mtoto ambaye aliyekuwa ameachwa katika hospitali ya Mama Lucy .
Korti imewaweka rumande watatu hao katika kituo cha polisi cha kileleshwa hadi novemba tarehe 23 wakati kesi hiyo itakapotajwa .