Vita dhidi ya Ugaidi

Uingereza kuipa Kenya Pauni milioni 9 kupambana na Al shabaab

Raab baadaye jumatano atakutana na waziri wa afya wa Kenya Muytahi Kagwe ili kujadiliana kuhusu jinsi Kenya itakavyopata chanjo ya Corona Oxford-Astrazeneca .

Muhtasari
  •  Raab baadaye jumatano atakutana na waziri wa afya wa Kenya Muytahi Kagwe ili kujadiliana kuhusu jinsi Kenya itakavyopata  chanjo ya Corona Oxford-Astrazeneca .
  •  Pia  atakagua majaribio ya utoaji wa chanjo hiyo huo Kilifi . Raab yuko nchini kwa ziara ya siku moja .
Dominic Raab ,waziri wa mashauri ya kigeni wa Uingereza na waziri wa mashauri ya kigeni wa Kenya Raychelle Omamo

 Waziri wa mashauri ya kigeni wa Uingereza  Dominic Raab  ametangaza kwamba nchi yake itaipa Kenya pauni milioni 9 ili kupiga jeki vita vyake dhidi ya kundi la kigaidi la al shabaab .

  Kenya pia itanufaika na  pauni milioni 48 za kuisadia kufadhli miradi ya kupmabana na mabadiliko ya hali ya anga  hasa katika maeneo  ambako athari za mageuzi ya hali ya anga yameziathiri jamii  kwa kusababisha kiangazi na mafuriko .

 Raab baadaye jumatano atakutana na waziri wa afya wa Kenya Muytahi Kagwe ili kujadiliana kuhusu jinsi Kenya itakavyopata  chanjo ya Corona Oxford-Astrazeneca .

 Pia  atakagua majaribio ya utoaji wa chanjo hiyo huo Kilifi . Raab yuko nchini kwa ziara ya siku moja .