Chanjo ya corona kwa wanawake wajawazito

Chanjo ya Moderna haifai kupewa wanawake wajawazito WHO yaonya

Dozi mbili ya Moderna inatarajiwa kukabiliana na aina yoyote itakayochipuka ya virusi hivyo ,kampuni hiyo imesema .

Muhtasari
  • WHO pia imesema watu ambao miili yao inaweza  kujibu vibaya viungo vyovyote vya chanjo hiyo hawafai  kuitumia  chanjo hiyo au chanjo yoyote ya   mRNA.
  •  Chanjo hiyo pia haifai kupewa watu walio  chini ya umri wa miaka 18  hadi matokeo ya utafiti Zaidi yatolewe .

 Shirika la afya duniani WHO limeonya kuwa chanjo ya Corona ya  moderna haifai kupewa wanawake walio wajawazito .

 Hakuna majaribio ya chanjo hiyo yaliofanywa kwa wanawake walio na uja uzito  na hayatarajiwi kufanywa  hadi robo ya kwanza ya mwaka wa 2021 ,WHO imesema

" Ingawaje  uja uzito unawaeka hatarini wanawake kukumbwa na covid 19  matumizi ya chanjo hii kwa wanaotarajia kupata watoto hayafai ..’ WHO imesema kupitia taarifa .

 Mkurugenzi wa chanjo Kate O'Brien  amesisitiza kwamba majaribio ya chanjo ya Moderna kwa wanawake waja wazito yanahitajika kwa wanawake walio na mimba .

" Hakuna  sababu ya kufikiria kwamba kuna tatizo  la  kuwa na uja uzito  tunakiri tu kwamba   maelezo hayapa kwa sasa’ amesema

WHO pia imesema watu ambao miili yao inaweza  kujibu vibaya viungo vyovyote vya chanjo hiyo hawafai  kuitumia  chanjo hiyo au chanjo yoyote ya   mRNA.

 Chanjo hiyo pia haifai kupewa watu walio  chini ya umri wa miaka 18  hadi matokeo ya utafiti Zaidi yatolewe .

 Siku ya jumatatu  Moderna Inc  ilisema chanjo yake inatoa  chembe za  kukabiliana na virusi vya Corona dhidi ya aina mpya ya virusi vya ugonjwa huo vilivyogundulika nchini Uingereza na Afrika Kusini .

 Dozi mbili ya Moderna inatarajiwa kukabiliana na aina yoyote itakayochipuka ya virusi hivyo ,kampuni hiyo imesema .