- Serikali kwa sasa inatoa huduma za bure za upangaji uzazi katika vituo va afya vya umma .
- Hata hivyo bado kuna ukosefu wa usawa katika kupata huduma za njia za kupanga uzazi kwani asilimia 1806 ya wanawake wanataka kuzitumia lakini hawawezi kuzifikia huduma hizo .
Takriban wanawake na wasichana milioni sita nchin Kenya wanatumia njia za kisasa za upangaji uzazi ili kuzuia kupata uja uzito ripoti mpya imeonyesha .
Idadi hiyo ni milioni 2 zaidi ya wanawake na wasichna milioni nne waliokuwa wakitumia njia za kupanga uzazi mwaka wa 2012 .
Katika mwaka mmoja uliopita wanawake hao wote na wasichana walizuia mimba milioni 2.2 zisizohitajika na kuepuka kuavya mimba 503,000 kwa njia isio salama kulingana na ripoti hiyo .
Ripoti hiyo iliyotolewa kwa ushirikianao wa mashirika ya UNFPA, USAID, the Bill & Melinda Gates Foundation na afisi ya Uingereza kuhusu maendeleo ya jumuiya ya madola iligundua kwamba Kenya ni miongoini mwa mataifa ambayo wanawake wake wengi wanatumia njia za kupanga uzazi barani Afrika
Ripoti hiyo inaonyesha kwamba asilimia 57.8 ya wanawake walioolewa wapo chini ya mpango wa upangaji uzazi . Hata hivyo ukijumuisha idadi ya wanawake wote wakiwemo wasio katika ndoa idadi hiyo inapungua hadi asilimia 42.5 . Kenya ilikuwa miongoni mwa nchi za kwanza kujitolea kuhusika na mpango wa FP 2020 ulipozinduliwa mwaka wa 2012.
Idadi ya sasa ya asilimia 57.8 ni upungufu mdogo kutoka asilimia 59 iliyosajiliwa mwaka wa 2018 ya idadi ya wanawake na wasichana wanaotumia njia za kisasa za upangaji uzazi .
Serikali kwa sasa inatoa huduma za bure za upangaji uzazi katika vituo va afya vya umma .
Beth Schlachter, mkurugenzi mkuu wa ameisifu Kenya kwa juhudi zake katika kuhakikisha kwamba huduma hizo zinapatikana kwa urahisi na bure . amesema hali iliboreshwa hata Zaidi wakati wa janga la Corona .
Hata hivyo bado kuna ukosefu wa usawa katika kupata huduma za njia za kupanga uzazi kwani asilimia 1806 ya wanawake wanataka kuzitumia lakini hawawezi kuzifikia huduma hizo .
Beth ameongeza : “ kila siku unapopita kuna mamilioni ya wanaotaka kutumia njia za kupanga uzazi ili kuamua hatima zao . Tunapoelkea mwaka wa 2030 tunafaa kuendelea na jitihada za kuboreka na kujenga msingi kutumia vinavyofanya vyema ili kuhakikisha kwamba hakuna msichana anayeachwa nyuma’
Nchini Kenya mbinu za kupanga uzazi kutumia sindano ndizo zinazopendelea kwa asilimia 47.9 ikifuatwa na ile ya vibandiko vikiwa na asilimia 18.2 ,tembe zikiwa nafasi ya tatu kwa asilimia 14.1, kuondolewa yao la uzazi kwa asilimia 5.6 na mbinu njia ya Lactational Amenorrhea Method (njia ya kumnyonyesha mtoto) kwa asilimia 0.3