Jamaa kutoka Vihiga ataka kumchumbia Ngina Kenyatta

Muhtasari

• Shem alisema alimaanisha kila neno katika shairi lake la mapenzi, na binti ya Rais ni mboni ya jicho lake.

• Anapenda utu na umaridadi ulioonyeshwa na Ngina Kenyatta katika hafla  ambazo ameonekana katika umma.

ngina-kenyatta2
ngina-kenyatta2

Shem Mukalo, mtoto wa mkata miwa huko Vihiga, aliwasisimua Wakenya kwa kumwaga mapenzi yake kwa Ngina Kenyatta.

Kijana wa miaka 30 kutoka Vihiga alianza kujulikana baada ya kuandika barua ya mapenzi kwa Ngina Kenyatta mwenye umri wa miaka 31.

Katika mazungumzo ya kipekee na ‘Word Is’ Shem alisema alimaanisha kila neno katika shairi lake la mapenzi, na binti ya Rais ni mboni ya jicho lake.

"Watu walikuwa wakiniambia kuwa maafisa wa ujasusi watanijia. Lakini niliwaambia hii ni barua tu ya kusherehekea mwanamke mzuri, sijamnyanyasa mtu yeyote. Kwanini niogope?

ngina
ngina

Wao ni wanadamu tu kama mimi. Dhamira yangu iko sawa kwa sababu nilikuwa nikimthamini tu mwanamke mzuri, "alisema.

Alisema barua yake ya mapenzi kwa Ngina ilikuja baada ya kuachana na mpenzi wake, na kwake, binti ya Rais ndiye mwanamke bora.

Anapenda utu na umaridadi ulioonyeshwa na Ngina Kenyatta katika hafla  ambazo ameonekana katika umma.

"Nina shisia za kimapenzi kwake. Najua vizuri kwamba hiyo ni kulenga ngumi kuliko uwezo wangu wangu kwa sababu anatoka kwenye familia tajika," alisema.

"Ikiwa itajiri mapema, ni vizuri. Nina matumaini tu. Ninajua pia ukweli kwamba huenda ndoto yangu isitimie. Niko tayari kwa baya zaidi. "

Alisema yuko tayari kukutana na Rais Uhuru Kenyatta. 

"Ikiwa sikutaka kuwa naye kama baba mkwe wangu, nisingejisumbu kuandika barua hiyo ya mapenzi."

Katika barua yake ya mapenzi, Shem aliahidi kumchukua Ngina kwenye ziara ya ulimwengu. Lakini ana pesa?

Ngina
Ngina

"Mimi ni mtu mwenye maono wengi. Hali yangu kwa sasa haiwezi kuwa nzuri kifedha. Labda ningeweza kumchukua kote ulimwenguni kama sasa, lakini katika kipindi cha miaka michache, naamini nitakuwa nimekusanya fedha kwa bidii yangu. "

Mamake alikuja kufahamu kuhusu barua yake aliomwandikia Ngina mnamo Juni 14, siku chache baada ya kuiandika. Alikuwa na wasiwasi kuhusu usalama wa mtoto wake baada ya kukiri upendo kwa mtu wa jamii ya hali ya juu.

Shem alisema hajali ukweli kwamba Ngina Kenyatta anazidi umri kwa mwaka mmoja . Kwake, umri ni idadi tu na sio suala katika harakati zake za kupata mchumba.

Kwa kuongezea, alisema wasichana wamekuwa wakimiminika ukurasa wake wa facebook tangu barua yake kali kwa binti ya Rais.