- Dennis Itumbi apatikana amepigwa kikatili muda mfupi baada ya kudaiwa kutekwa nyara
Mwanablogu na mshirika wa karibu wa DP William Ruto Dennis Itumbi amepatikana akiwa hai baada ya kudaiwa kutekwa nyara jana (Alhamisi) alipokuwa akitoka kwenye kinyozi.
Ripoti kwenye mitandao ya kijamii zilifichua kuwa Itumbi alitekwa nyara na kuwekwa ndani ya gari ambalo lilitoweka bila kujulikana.
Kulikuwa na madai kuwa alikamatwa kwa kukosa kuheshimu wito wa mahakama kuhusu kesi yake ya matunzo ya mtoto.
Hata hivyo, mamlaka ya polisi hata hivyo ilikanusha kuwa mwanablogu huyo alikuwa chini ya ulinzi wao.
Kulingana na Seneta wa Elgeiyo Marakwet Kipchumba Murkomen, Itumbi alipatikana amepigwa kikatili na kwa sasa anapokea matibabu hospitalini.
“Nimefurahi kumuona ndugu yetu Itumbi akiwa hai. Inasikitisha kumuona akiwa katika maumivu hayo. Natumai kwamba atarudi kwa nguvu zaidi. Alishtushwa na maafisa wa Polisi ambao wanapaswa kumlinda walimdhuru. Watesi wake wanaofurahia madaraka wasijue amani. Siasa hazifai kufanywa hivi,” Murkomen aliandika kwenye Twitter.
Glad to see our brother @OleItumbi alive. Sad to see him in such pain. Hopeful that he will bounce back stronger. Appalled that Police officers who should be protecting him harmed him.May his tormentors who are enjoying power never know peace. Politics shouldn’t be done this way. pic.twitter.com/tz97ANcA2g
— KIPCHUMBA MURKOMEN, E.G.H (@kipmurkomen) December 23, 2021
My brother has been badly beaten. We thank God that he is alive. On his own account he was arrested by police and beaten and tortured. This is the state we found him in. (See pictures) Please pray for his recovery. Asanteni for your many prayers and support pic.twitter.com/tXBmfHZPfM
— David Itumbi (@ItumbiDavid) December 23, 2021