•Habari za kuhama kwake zilitangazwa kwenye ukurasa wa Twitter, Jumatatu asubuhi, na chama cha UDA .
•Hatua ya Jaguar inajiri siku chache baada ya mcheshi Jasper Muthomi, almaarufu Mc Jessy, kutangaza kuwa atawania kiti cha Imenti Kusini kwa tikiti ya chama cha UDA
Mbunge wa Starehe Chalres Njagua almaarufu Jaguar amejiunga rasmi na chama cha Naibu Rais William Ruto, UDA.
Habari za kuhama kwake zilitangazwa kwenye ukurasa wa Twitter, Jumatatu asubuhi, na chama hicho .
"The Hustler Nation inamkaribisha Mhe. Charles Kanyi Njagua Mbunge wa Starehe. Chama kinazidi kukua kwa kasi na mipaka huku viongozi wengi wakichagua kujiunga na kikosi cha washindi."
Hatua ya Jaguar inajiri siku chache baada ya mcheshi Jasper Muthomi, almaarufu Mc Jessy, kutangaza kuwa atawania kiti cha Imenti Kusini kwa tikiti ya chama cha UDA.
Mcheshi huyo alithibitisha Jumatano kwamba amejiunga rasmi na chama kinachongoozwa na Ruto baada ya mashuriano mapana na wakazi wa eneo hilo.