Bruno Shioso:Huduma ya Polisi iko imara kuzuia shambulio lolote

Muhtasari

•Ameleeza ameimarisha  ulinzi kote nchini na wamejipanga vyema kudhibiti shambulio lolote linalopangwa na wahauni

•Kauli hiyo inajiri saa chache baada ya Ufaransa kuwataka raia wake walio nchini Kenya kuwa waangalifu wanapozuru maeneo ya umma kwani kuna hatari ya kulenga maeneo ya umma yanayotembelewa na raia wa kigeni, haswa jijini Nairobi

Inspekta Jenerali wa Polisi Hillary Mutyambai.
Inspekta Jenerali wa Polisi Hillary Mutyambai.
Image: HISANI

Huduma ya Kitaifa ya polisi(NPS) imevunja kimya baada taarifa iliyotolewa na  nchi za kigeni  kwamba Raia wake ambao wanaishi humu nchini wajiepusha na baadhi ya sehemu  humu nchini. 

Msemaji wa Polisi  Bruno Shioso ameeleza kuwa polisi wameimarisha  ulinzi kote nchini na wamejipanga vyema kudhibiti shambulio lolote linalopangwa na wahauni.

"Idara yetu imehakikisha shughuli za usalama zinapewa  kipaumbele, ambapo tutahakikisha kuwa hakuna mashambulizi  yote yatazuiliwa,"  alisema Bruno Shioso.

Kauli hiyo inajiri saa chache baada ya Ufaransa kuwataka raia wake walio nchini Kenya kuwa waangalifu wanapozuru maeneo ya umma kwani kuna hatari ya kulenga maeneo ya umma yanayotembelewa na raia wa kigeni, haswa jijini Nairobi.

Katika taarifa iliyotolewa Alhamisi, Ufaransa ilisema kuwa mikahawa, hoteli, sehemu za burudani , vituo vya ununuzi ni miongoni mwa maeneo yaliyolengwa ambayo yanapaswa kuepukwa na raia wake.