Uchaguzi 2022: Orodha ya maseneta waliochaguliwa tena

Katika uchaguzi wa mwaka huu, maseneta wengi walihifadhi viti vyao.

Muhtasari

Katika uchaguzi wa mwaka huu, maseneta wengi walihifadhi viti vyao.

MASENETA
MASENETA
Image: WILLIAM WANYOIKE

Wakenya mnamo Jumanne, Agosti 9, walitekeleza wajibu wao wa kiraia kwa kuwapigia kura wagombeaji waliowapendelea kutoka urais hadi wabunge wa bunge la kaunti.

Kaunti zote 47 zilishiriki katika kuchagua seneta wao ajaye.

Baadhi ya wagombea walihifadhi viti vyao huku wengine wakishindwa, kama ilivyo kawaida katika kila uchaguzi

Hii hapa orodha ya Maseneta wateule:

Kaunti ya Migori

Mgombea wa ODM Eddy Oketch alipata kura 295,228, na kushinda kiti hicho.

Kaunti ya Busia

Mgombea wa chama cha NRA Okiya Omtatah alishinda kwa kura 171,681.

Hillary Itela wa ODM aliibuka wa pili kwa kura 59,276.

Kaunti ya Homa Bay

Moses Kajwang' wa ODM amehifadhi kiti chake baada ya kupata kura 353,882. Mpinzani wake wa KANU Thomas Ojanga alipata kura 18,690.

Kaunti ya Kisumu

Tom Ojienda wa ODM amejinyakulia kiti hicho kwa kura 413,121. Enos Kudi Okolo wa Jubilee aliibuka wa pili kwa kura 15,575.

Kaunti ya Bungoma

Ford Kenya Moses Wetang'ula amehifadhi kiti chake cha useneta wa Bungoma. Alipata kura 286,143.

Kaunti ya Pokot Magharibi

Mgombea wa chama cha UDA Julius Murgor alishinda kwa kura 72,240.

Kaunti ya Trans Nzoia

Mgombea wa chama cha UDA Allan Chesang amejinyakulia kiti hicho kwa kura 123,793.

Kaunti ya Uasin Gishu

Mgombea wa chama cha UDA Jackson Mandago amejinyakulia kiti hicho kwa kura 252,800.

Kaunti ya Kakamega

Mgombea wa chama cha UDA Boni Khalwale amejinyakulia kiti hicho kwa kura 247,860.

Kaunti ya Bomet

Mgombea wa chama cha UDA Hillary Sigei, amejinyakulia kiti hicho kwa kura 237,192. Enock Kemei wa CCM alipata kura 57,745 huku Weldon Korir akipata kura 41,106.

Wilaya ya Siaya

Mgombea wa chama cha ODM Oburu Odinga amenyakua kiti hicho kwa kura 285,595. Julius Okinda Okinda, mgombea binafsi, aliibuka wa pili kwa kura 33,898.

Tharaka Nithi

Mgombea wa chama cha UDA Mwenda Gataya amejinyakulia kiti hicho kwa kura 71,246. Samwel Ragwa, chama huru alichukua nafasi ya pili kwa kupata kura 46,205.

Kaunti ya Kwale

Issa Boy wa ODM alihifadhi kiti chake baada ya kupata kura 52,772. Katika nafasi ya pili alikuwa Antony Yama wa UDA aliyepata kura 41,762.

Kaunti ya Mombasa

Faki Mwinyihaji amehifadhi kiti chake kwa kutumia tiketi ya ODM baada ya kupata kura 11,040. Alimwangusha Hamisi Mwaguya wa UDA ambaye alikuwa na kura 76,069.

Kaunti ya Taita Taveta

Jones Mwaruma wa ODM alimshinda mpinzani wake wa karibu na MCA anayeondoka wa Sagala Godwin Kilele wa Jubilee kwa kura 39,142. Kilele alifanikiwa kupata kura 26,158.

Kaunti ya Narok

Gavana wa sasa Ledama Olekina amefanikiwa kutetea kiti chake baada ya kuzoa kura 135,108. Alimshinda Gavana Aliyeondoka Samuel Tunai aliyepata kura 117,869.

Kaunti ya Makueni

Mbunge anayeondoka wa Makueni Daniel Maanzo wa Wiper ameshinda kwa kura 177,273. Gavana anayeondoka Kivutha Kibwana, kiongozi wa chama cha Muungano alipata kura 59,034.

Kaunti ya Laikipia

Mgombea wa UDA John Kinyua alitetea kiti chake baada ya kupata kura 59,947.

Kaunti ya Kitui

Seneta wa sasa Enock Wambua amehifadhi kiti chake baada ya kujizolea kura 191,317.

Mgombea wa Wiper alimwangusha Stephen Kilonzo wa UDA, aliyepata kura 49,064.

Kaunti ya Kiambu

Karungo Thang’wa wa UDA ameshinda kiti hicho baada ya kujizolea kura 579,411.

George Maara wa Jubilee aliibuka wa pili kwa kura 112,304.

Kaunti ya Nairobi

Katibu mkuu wa chama cha ODM Edwin Sifuna ameshinda kiti hicho kwa kura 716, 876 huku mshindani wake wa karibu Askofu Margret Wanjiru wa UDA akiibuka wa pili na kura 554,091.

Matokeo zaidi yanafuata...