Mwalika wa Wiper ahifadhi kiti chake cha ubunge wa Kitui-Rural

Mpinzani wake wa pekee Charles Nyamai wa UDA alipata kura 10,178.

Muhtasari

•Mwalika alipata kura 19,735 na kumshinda mpinzani wake wa pekee Charles Nyamai wa UDA ambaye alipata kura  10,178.

David Mwalika apokea cheti kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi wa Kitui-Rural Winfred Ndoti baada ya afisa huyo kumtangaza kuwa mshindi wa uchaguzi wa Jumatatu.
David Mwalika apokea cheti kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi wa Kitui-Rural Winfred Ndoti baada ya afisa huyo kumtangaza kuwa mshindi wa uchaguzi wa Jumatatu.
Image: MUSEMBI NZENGU

David Mwalika wa chama cha Wiper amehifadhi kiti chake cha ubunge katika eneo la Kitui-Rural.

Mwalika alipata kura 19,735 na kumshinda mpinzani wake wa pekee Charles Nyamai wa UDA ambaye alipata kura  10,178.

Katika matokeo ya uchaguzi ambayo yalitangazwa na msimamizi wa uchaguzi wa eneo bunge Wilfred Ndoti katika kituo cha kuhesabia kura Kusini Mashariki mwa Kenya, saa nane asubuhi Jumanne asubuhi.

Jumla ya kura zilizopigwa ni 33, 089 kati ya 55,000 waliojiandikisha.

Katika hafla iliyoshuhudiwa na msimamizi wa uchaguzi katika Kaunti ya Kitui, Macharia Gichichi Ndoti, alitangaza kuwa kura 166 ziliharibika.

Aliweka idadi ya wapiga kura kuwa asilimia 54.7.

Aliyekuwa karibu kushuhudia Mwalika akikabidhiwa cheti cha ushindi ni mwenyekiti wa kundi la wabunge wa UKambani Benson Makali Mulu ambaye pia ni mbunge wa Kitui ya kati.

Wengine waliohudhuria ni seneta wa Kitui Enoch Wambua na mbunge wa kaunti hiyo katika bunge la kitaifa.

Mbunge wa Mwingi Kaskazini Paul Nzengu na mwenzake wa Mwingi magharibi Charles Nguna pia walikuwepo.