Facebook inawadhuru watoto na kudhoofisha Demokrasia, asema mfanyakazi wake wa zamani

Muhtasari

•Frances Haugen, mwenye umri wa miaka 37, meneja wa zamani wa bidhaa katika kampuni ya Facebook aligeuka kuwa mfichua siri, ambaye ameikosoa sana kampuni katika bunge la congress la Marekani.

•Facebook imekuwa ikikosolewa kwa kila kitu kuanzia kushindwa kulinda usiri wa watumiaji hadi kutofanya juhudi za kutosha kuzuwia usambaaji wa taarifa potofu.

Image: HISANI

Mfanyakazi wa zamani wa Facebook amewaambia wabunge nchini Marekani kwamba tovuti na programu za kampuni hiyo ’’zinawadhuru watoto, zinasababisha mgawanyiko na kuthoofisha demokrasia yetu ".

Frances Haugen, mwenye umri wa miaka 37, meneja wa zamani wa bidhaa katika kampuni ya Facebook aligeuka kuwa mfichua siri, ambaye ameikosoa sana kampuni katika bunge la congress la Marekani.

Frances Haugen alikuwa mfanyakazi wa zamani wa kampuni ya Facebook
Frances Haugen alikuwa mfanyakazi wa zamani wa kampuni ya Facebook
Image: BBC

Facebook imekuwa ikikabiliwa na uchunguzi na ongezeko la miito inayoitaka idhibiti mtandao huo.

Facebook imesema nini?

Muasisi wa Facebook Mark Zuckerberg amejibu, akisema, maelezo ya hivi karibuni yalitoa "picha ya uongo" kuihusu kampuni.

Image: FACEBOOK// MARK ZUCKERBERG

Katika barua yake kwa wafanyakazi, amesema kuwa mengi kati ya madai ‘’hayana maana yoyote’’ huku akielezea juhudi zao katika kupambana na maudhui yenye madhara, kuanzishwa kwa uwazi na kubuni " mpango wa tafiti unaoongozwa na kampuni hiyo kushugulikia masuala haya ".

’’Tunajali sana kuhus masuala kama usalma, maisha bora na afya ya akili’’, amesema Bw Zuckerberg, katika barua yake iliyowekwa kweney ukurasa wake wa Facebook.

"Ni vigumu kusikia maelezo ambayo hayawakilishi kazi yetu na nia zetu’’

Facebook ni mtandao maarufu zaidi wa kijamii duniani. Kampuni inasema ina watumiaji bilioni 2.7 wanaotembelea ukurasa huo kila.

Mamia ya mamilioni ya watu pia hutumia mitando mingine ya kamouni hiyo, ikiwa ni pamoja na WhatsApp na Instagram.

Lakini imekuwa ikikosolewa kwa kila kitu kuanzia kushindwa kulinda usiri wa watumiaji hadi kutofanya juhudi za kutosha kuzuwia usambaaji wa taarifa potofu.