Ni miezi miwili imepita tangu mwanamuziki kutoka Tanzania, Harmonize kumtambulisha hadharani mpenzi wake Briana.
Harmonize, akiwa ziarani nchini Marekani, mwishoni mwa mwezi Novemba, 2021 , alijipata kwenye mahaba mazito na mrembo kutoka Austria.
Alipotua uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere aliwaahidi mashabiki wake kwamba mwaka ujao, yaani 2022, atafunga ndoa naye.
Hivi majuzi Harmonize alitania mashabiki wake kwamba wameachana na kipenzi chake cha roho, Briana, jambo ambalo alikuja kueleza ulikuwa uwongo.
Baada ya Briana kuzuru Tanzania, Harmonize alimpeleka moja kwa moja kwa wazazi wake kumtambulisha rasmi, mkoani Mtwara.
Harmonize kwenye kituo kimoja cha runinga ameeleza kuwa anapanga kuasi ukapera mwaka huu na anapania kumwalika Ali kiba kutumbuiza kwenye harusi yake.
“Briana ndiye mwanamke wa maisha yangu!” alisema Harmonize.
Briana ni mwanamke wa pili mwenye asili ya kizungu kuwa kwenye uhusiano na Harmonize baada ya kuachana Sarah Michelloti raia wa Italia.