•Maggie amekuwa wa hivi majuzi kutangaza kuwa atakuwa kwenye kinyanganyiro cha mwakilishi wa kike kaunti ya Nairobi.
• Maggie anajulikana zaidi kwenye kipindi cha runinga 'Maria' ambacho kilikuwa peperushwa na runinga ya citizen mwaka jana.
Muigizaji nchini Kenya Dorea Chege, almaarufu Maggie amekuwa wa hivi punde kutangaza kwamba atakuwa kwenye kinyanganyiro cha mwakilishi wa kike kaunti ya Nairobi.
Maggie anajulikana zaidi kwenye kipindi cha runinga 'Maria' ambacho kilikuwa peperushwa na runinga ya citizen mwaka jana.
Kupitia ukurusa wake wa Instagram ameeleza kwamba atakuwa anagombea kiti cha mwakilishi wa kike Kaunti ya Nairobi akiwa mgombea huru.
Dorea amejiunga na wasanii mbali mbali ambao wametangaza rasmi kuwa watakuwa debeni Agosti mwaka huu liwe liwalo.
Baadhi ya watu mashuhuri nchini Kenya ambao wametangaza wazi kuwa watakuwa debeni ni ikiwemo Jalang'o, Mc Jessyi, Rufftone na Prenzo.