•Mshawishi wa mitandao na mfanyabiashara,Mylee Staicey amefunguka na kueleza kuwa Kilichosabisha mahusiano ya na mwimbaji wa injili Weezdom kufikia tama
•Alieleza kuwa alikuwa ameonywa kuchumbiana na mwimbaji huyo lakini licha ya onyo zote hizo ziliambulia patupu
Mshawishi wa mitandao na mfanyabiashara,Mylee Staicey amefunguka na kueleza kuwa Kilichosabisha mahusiano yake na mwimbaji wa injili Weezdom kukatika.
Staicy Mylee ametangaza azma ya kuwania kiti cha ubunge cha Kibwezi kwenye uchaguzi ujao wa tarehe 9 Agosti.
Staicey alianza kuwa mshawishi wa mitandao akiwa bado mwanafunzi,lakini hakuwa na matarajio ya kujulikana haraka kama ilivyotokea.
Kupitia mahojiano na kituo cha radio moja humu nchini alieleza kuwa walipatana na Weezdom kwenye hafla moja, Kaunti ya Kiambu ambapo alikuwa amepeleka rafiki yake.
Alieleza kuwa alikuwa ameonywa kuchumbiana na mwimbaji huyo lakini onyo zote ziliambulia patupu, baada ya hapo alieleza Weezdom alimtamfuta kwenye ukurusa wa instagram na mapenzi yao yakaanza kuota.
"Tulikutana wakati wa hafla moja huko Kiambu, rafiki yangu na Weezdom walijuana kwa hivyo utambulisho ulianza,”Alisema Mylee Staicey.
Vilevile, alieleza kama si mahusiano yake na Weezdom asingeweza kutambulika humu nchini kwa kasi kama ilivyotokea.