• Miezi mitatu iliyopita mchekeshaji Eric Omondi na mpenzi wake wa muda mrefu Lynn walikuwa na hamu ya kutarajia mtoto wao wa kwanza.
Siku chache baada mchekeshaji na mwanablogu Eric Omondi kufichua kuweka wazi sura ya bintiye mitandaoni hatimaye ameweka wazi sura ya bintiye wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwenye ukurasa wake wa instagram.
Alhamisi hii Eric alichapisha picha za bintiye kuonesha uso wa bintiye, Kyla, kwa ulimwengu, Ufichuzi huo, uliogubikwa na matarajio mengi kutoka kwa wafuasi wao hakika umepokelewa vyema na wanablogu wa mitandao.
Itakumbukwa miezi mitatu iliyopita kabla ya mwanawe kuzaliwa, Omondi alikuwa ameweka wazi kwamba asingeweka sura ya bintiye mitandaoni pasi na mtu kutoa kima cha shilingi milioni 50.
"Kufichua uso wa mtoto wangu haitakuwa rahisi," Omondi alisema. “Ili niweze kuonesha uso wa mtoto wangu, nitahitajika kulipwa Ksh 50 milioni. Atakayetoa kiasi hicho, ndiye atakayeonyesha sura yake. Uso wa mtoto wangu ni adimu sana na wa thamani.”
Miezi mitatu iliyopita mchekeshaji Eric Omondi na mpenzi wake wa muda mrefu Lynn walikuwa na hamu ya kutarajia mtoto wao wa kwanza miezi michache baada ya kutangaza kuharibikiwa na mimba yao ya kwanza.